Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaipongeza Wizara kupitia Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa ya kusimamia Wizara hii. Natambua Waziri alifika katika Jimbo langu la Iramba ya Mashariki na kuona tatizo la maji na jinsi watu wanavyohangaika, hii ni tofauti na mifugo. Ninashauri yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ukaguzi kwa mradi wa uchimbaji visima katika vijiji kumi pesa ambazo zilitolewa na Serikali lakini baadhi ya visima havina maji ya kutosha na pesa zimelipwa. Serikali ione namna ya kujenga na kutoa fedha kwa ajili ya mradi huo wa visima kumi. Pia Serikali ione namna ya kusaidia Wilaya kame kupata malambo na mabwawa ikiwemo Mkalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Makao Makuu ya Wilaya ya Mkalama ni Nduguti, mji ambao hauna maji. Naomba Wizara ione namna ya kuanzisha mradi maalum katika Makao Makuu ya Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imetoa shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya Kinyambuli, ni muhimu mradi wa maji ukapelekwa kwenye kituo hiki cha afya.