Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Ulanga imekuwa na ongezeko kubwa la mifugo kutokana na kuwa na eneo zuri kwa ajili ya malisho pamoja na migogoro inayoendelea katika wilaya za jirani kati ya wakulima na wafugaji. Hivyo, naiomba Serikali, kwanza kuchukua hatua za dharura kwa ajili ya kuweka mazingira bora kwa ajili ya wafugaji ili kuweza kujenga majosho na marambo kuepusha wafugaji hawa kutohamahama kwani katika wilaya yangu japo huwa kuna ng‟ombe zaidi ya 20,000 lakini hakuna huduma hata moja ya mifugo. Pia kuipatia usafiri Idara ya Mifugo ili iweze kutoa huduma kama chanjo kwa mifugo hiyo na kutoa huduma kwa urahisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ambayo yana mifugo mingi mpaka sasa ni yafuatayo:-
(i) Kata ya Iragua – ng‟ombe zaidi ya 6,000 hakuna majosho;
(ii) Kata ya Lukande – ng‟ombe zaidi ya 4,000 hakuna huduma yoyote;
(iii) Kata ya Mawimba – ng‟ombe zaidi ya 3,000 hakuna huduma yoyote;
(iv) Kata ya Milola – ng‟ombe zaidi ya 4,000 hakuna huduma yoyote; na
(v) Kata ya Uponera – ng‟ombe zaidi ya 2,000 hakuna huduma yoyote.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Ulanga kuna miradi mingi ya kilimo cha umwagiliaji lakini hakuna hata mradi mmoja uliokamilika. Hivyo, naiomba Serikali kunipa majibu ni lini miradi hiyo ya umwagiliaji itakamilika ili iweze kusaidia kuinua uchumi wa wananchi wa Ulanga?
Mheshimiwa Naibu Spika, uvuvi; Wilaya ya Ulanga tuna Mto wa Kilombero lakini watu wanaoishi kuzunguka mto huo hawajawezeshwa namna bora ya kufanya uvuvi na kupelekea uvuvi haramu ambapo kumeleta uhaba wa samaki. Hivyo, naiomba Serikali kuweka mpango mzuri ili watu wanaoishi maeneo ya mto wafaidike na uvuvi.