Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Wizara hii muhimu kwa uhai wa wananchi wetu. Nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa uhai na uzima hata tumefika jioni hii ya leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Wizara kwa kazi ya utekelezaji wa miradi ya maji katika jimbo langu na ziara ya Mheshimjiwa Waziri na Naibu wake kafika katika jimbo langu kuona changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama na miradi ya maji ya umwagiliaji. Naomba Serikali kutupatia fedha za ukarabati na upanuzi wa miradi ya maji ya vijiji vya Mkuyuni, Pangawe na Kizinga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Mkuyuni ni mradi chakavu na wa muda mrefu, tangu mwaka 2000 wakati huo mahitaji ni madogo na watu wachache. Naomba Serikali kutenga fedha za ujenzi wa tenki kubwa, kubadilisha mabomba kutoka nchi nne na kuweka ya nchi sita na kujenga kidaka maji kipya juu zaidi ya chanzo, ili kuwe na msukumo mkubwa zaidi kuwezesha maji kufika katika vitongoji vyote na kijiji cha Kivuma ambacho kipo juu zaidi ya Mkuyuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba upanuzi wa Mradi wa Maji wa Pangawe na Kizinga na ukarabati mkubwa, kwa sababu mahitaji ya maji yameongezeka, uelewa wa watumia maji safi na salama umeongezeka, idadi ya watu imeongezeka na ujio wa viwanda katika kata hii ya Mkambarani kama vile cha Phillip Morris na Mahashree yanaongeza idadi ya watu na mahitaji kuongezeka. Naomba mahitaji ya vifaa kama vya mradi wa Mkuyuni na Kivuma ipatiwe fedha kwa mradi huu wa Pangawe pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu la pili ni kukipatia maji kijiji cha Mfumbwe kwa sababu wana chanzo cha maji ya msereko karibu, pia vijiji vyote vilivyozunguka vina maji kasoro kijiji hicho kimoja kilicho katika kata Mkuyuni.

Pia naomba Serikali itupatie fedha katika mradi wa umwagiliaji katika shamba la kijiji cha Kibwaya katika Bonde la Mto Kibwaya, Kisemu mpaka Mfumbwe ili kuwawezesha wakulima kulima zaidi ya mara moja kwa mwaka na kuongeza kipato cha wakulima na uhakika wa chakula katika kijiji hiki, Kata na Tarafa nzima ya Mkuyuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba Serikali kufanya ukaguzi maalum katika mradi wa umwagiliaji wa kijiji cha Kwika sababu umechukua muda mrefu tangu mwaka 2005 mpaka sasa. Pamoja na kutuma kiasi kikubwa cha fedha, lakini bado mradi haujamalizika na kujengwa chini ya kiwango na kupoteza fedha za umma.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja na mchango wangu uzingatiwe pamoja na ule wa mdomo.