Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninatoa masikitiko makubwa sana kwa ukosefu wa maji katika majimbo ya pembezoni ya Mkoa wa Iringa. Wananchi wanapata adha kubwa sana. Katika kitabu cha Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 271 namba 63, 65 na 66 jinsi ambavyo Wizara na watendaji wake wamefanya kazi ya ku–copy and paste kwani wameonesha visima hivyo vipo katika Mkoa wa Iringa wakati visima hivyo vipo Mkoa wa Njombe na si Iringa.

Mheshimiwa Naibu Spika, haya makosa yanasababisha adha kubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Iringa hasa Wilaya ya Iringa, Jimbo la Kalenga na Isimani ambapo kuna changamoto kubwa sana ya maji. Kuna shida kubwa ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa ya umwagliaji ya vijiji vya Ibumila na Mgama ambavyo vipo kata ya Mgama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kalenga kumekuwa na uchakavu wa miundombinu ya maji yote, hivyo tunaiomba Serikali itoe pesa wananchi wapate maji. Vivyo hivyo kata za Kihorogota na Kisinga vilivyopo Jimbo la Ismani vipatiwe maji.