Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa pongezi kwa umahiri wa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli pamoja na Waziri, Mheshimiwa Engineer Kamwelwe kwa umahiri wake katika kusimamia kazi za Wizara na miradi yake ili kumtua mama ndoo.

Pia pongezi kwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Wakurugenzi wa Maji Vijijini na Mijijini na watendaji wote katika Wizara. Pia pongezi kwa Wizara kubadili utaratibu wa malipo kwa hati kutumwa Wizarani badala ya kupeleka pesa katika Halmashauri ambazo ziliweza kubadilishwa matumizi au miradi kuchelewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mabonde ya maji; Mamlaka ya Mabonde bado yana changamoto za watumishi katika maeneo yanayotakiwa kusimamiwa ipasavyo. Hivyo nashauri Wizara ya Maji iangalie itahusisha vipi Halmashauri au Manispaa kusimamia kwa kutoa fedha za usimamizi ili kulinda vyanzo vya maji ambavyo vinavamiwa sana na wafugaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu banio katika Mto Katuma na Mto Mpanda Mkoa wa Katavi; Wilaya ya Mpanda, Kata za Itenka, Kakese na Mwanamkulu zinalima sana zao la mpunga hivyo kuna haja ya kupata skimu ya umwagiliaji ili kilimo kifanyike mara mbili kwa mwaka. Pia kuwekea mabanio ya kusambaza maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu chanzo Ziwa Tanganyika, Mkoa wa Katavi bado unategemea vyanzo ambavyo si vya uhakika, mfano, Manispaa ya Mpanda wanapata maji kutoka Ikorongo chanzo ambacho hakikidhi mahitaji. Hivyo tunaomba Wizara ifanye upembuzi yakinifu kwa ajili ya kutoa maji Ziwa Tanganyika na kutumika Wilaya mbili yaani Tanganyika na Mpanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la madeni ya miradi ya maji katika Halmashauri, kampuni ya kizalendo ya Kahama ilikopesha wakandarasi katika Halmashauri takribani kumi ikiwemo ya Nkasi ambayo kuna utata wa mkataba na vigezo ambapo kampuni mbili zinadaiwa takribani shilingi bilioni mbili. Naomba Serikali iingilie kati mgogoro huo ili kampuni hiyo iweze kulipwa madeni. Ahsante.