Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Maji. Pia ninaomba mchango wangu huu wote uingie kwenye Hansard.

Mheshimiwa Naibu Spika, maji ni uhai, suala la maji ni muhimu sana katika jamii. Miradi ya maji mingi inayotokana na World Bank ni miradi ambayo imetumia pesa nyingi sana na mingi haijakamilika. Ni kwa nini wahusika katika miradi hii ya maji ambayo haijatekelezeka hawachukuliwi hatua? Iko miradi zaidi ya minne ya fedha za World Bank ambayo haipo katika hali nzuri mkoani Ruvuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuainisha miradi ya maji iliyoko katika Mkoa wa Ruvuma ambayo haijakamilika na kimsingi fedha hizo hazijulikani ziliko kwa kuwa inaonesha fedha zimetumika na miradi haijakamilika kama ifuatavyo:-

(1) Mradi wa Maji Mkako katika Wilaya ya Mbinga ambao umetumia fedha zaidi ya shilingi 600,000,000;

(2) Mradi wa Maji wa Litola Wilayani Namtumbo umetumia fedha zaidi ya shilingi million 700,000,000; na

(3) Mradi wa Maji wa Matemanga Wilayani Tunduru (Tunduru Kaskazini) ambao umetumia fedha zaidi ya 500,000,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, ubadhirifu huu unaofanywa katika Wizara hii kwenye miradi hii ya maji hauvumiliki.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu iundwe Tume ya kufuatilia miradi hii ili tupate majibu sahihi juu ya miradi hii na ufisadi mkubwa uliopo kwenye miradi hiyo. Mimi nilikuwa Mjumbe wa Kamati ya LAAC ninajua vizuri juu ya miradi mbalimbali ya maji iliyoko katika nchi yetu katika mikoa ya Tanga, Mbeya, Iringa na maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.