Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi ya kuchangia kwenye Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuwapongeza Mawaziri, Waziri Kamwelwe ambaye ni Waziri pamoja na Naibu kwa sababu walifanya ziara kwenye Mkoa wangu wa Morogoro na walifanya ziara mpaka Malinyi, walifanya ziara Mlimba na Morogoro Mjini lakini ziara imefanyika ila bado kuna matatizo mbalimbali. Nashukuru Serikali kwa miradi ambayo tayari inatoa maji na kwa upande wa umwagiliaji ambayo tayari inafanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na mradi wa maji Morogoro Mjini. Mradi wa Maji Morogoro Mjini umechukua muda mrefu na hiki kilio tumekifikisha mpaka kwa Mheshimiwa Rais alipokuwa kwenye ziara Morogoro, naomba sana huu mradi uweze kumalizika kwa sababu unafadhiliwa na Wafaransa pamoja na Serikali ya Tanzania ambapo Serikali ya Tanzania kwenye bajeti hii imetenga shilingi bilioni nane pamoja na Euro. Naomba sana Waziri aione kuwa ni kazi kweli mradi huu wa maji Manispaa kukosa maji siyo vizuri sana. Kuna baadhi ya Kata ambazo hazipati maji kabisa zingine zinapata maji kwa mgao, kwa hiyo, naomba sana aifanyie kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wakala wa Maji Vijijini kama wenzangu walivyosema naomba na yenyewe ifanyiwe kazi na yenyewe iweze kuanzishwa. Miradi ya Benki ya Dunia ambayo haijamalizika iweze kumalizika. Miradi mingine ya umwagiliaji pamoja na maji viporo iweze kumalizika. Mradi wa Chalinze awamu ya tatu nao umechukua muda mrefu tatizo ni kuwa mkandarasi alisitisha mkataba, naomba ifanyiwe kazi ili kusudi uweze kuanza kwa sababu unatoa maji kwenye Mkoa wa Pwani, Kibaha pamoja na Morogoro kwenye vijiji vingine vya Morogoro kama Kidugalo.

Kwa hiyo, naomba na wenyewe ufanyiwe kazi uweze kufanya kazi, Mheshimiwa Waziri unajua kuwa umechukua muda mrefu naomba uweze kufanyiwa kazi. Bwawa la Kidunda naomba na lenyewe lifanyiwe kazi ni kweli limekuwa la muda mrefu lakini nashukuru naipongeza Serikali kwa sababu imetenga hela, kwa hiyo, hizo hela ziweze kusimamiwa na kuangaliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo cha umwagiliaji ndiyo muhimu kwa nchi yetu ya Tanzania kutokana na tabianchi. Ni asilimia 1.6 mpaka sasa hivi ambayo inamwagiliwa, lakini kuna mpango kabambe ambao umepangwa naomba ufuatwe na uweze kukamilika kusudi tuweze kupata kilimo cha umwagiliaji.

Pia naipongeza Serikali kwa miradi ya kilimo cha umwagiliaji ambayo inafanyika Mkoani Morogoro. Kwa mfano, kilimo cha mpunga ambacho kinafanyiwa Msolwa Stesheni, Ujamaa, scheme za Ludewa pamoja na Rumuma na zingine ambazo kwa bajeti hii zimetengewa shilingi bilioni 7.2, naomba hizi hela ziweze kutolewa na ziweze kusimamiwa vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye mteremko wa fedha, mteremko wa fedha wengi wameshachangia lakini naomba hasa kwenye fedha za maendeleo ambapo lazima miradi ya maji iweze kuisha, scheme za umwagiliaji ziweze kukamilika. Naomba hizo hela tunazotenga kwenye Bunge kama inawezekana naiomba Serikali yangu ziweze kupatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uvunaji wa maji kutokana na tatizo la tabianchi naomba tuweze kufuata uvunaji wa maji na hii sera iweze kufuatwa na kuwekewa mikakati kabisa pamoja na vyanzo vya maji viweze kutunzwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuomba sana tena sana miradi ya maji iweze kukamilika. Umenipatia dakika tano na point zangu nimeziongea kwenye dakika tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na ahsante sana.