Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. BALOZI. DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono haja. Katika ukurasa wa 63 hadi 64 wa hotuba ya Waziri imeandikwa ifuatavyo:-
“Katika mwaka 2015/2016 Wizara imesambaza na kutoa elimu kwa wadau kuhusu Sera ya Taifa ya Mifugo ya mwaka 2006 na Mkakati wa Taifa wa Kuendeleza Sekta ya Mifugo wa mwaka 2011. Jumla ya nakala 300 za Sera ya Taifa ya Mifugo na nakala 200 za Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Mifugo zimesambazwa”.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakala hizi ni kidogo ukizingatia umuhimu wa sekta ya mifugo. Nashauri nakala nyingi zaidi zichapwe na kusambazwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni Mheshimiwa Waziri Mkuu akifuatana na Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi alitembelea Kata ya Kakunyu-Missenyi na kutoa maelekezo ya jinsi ya kumaliza mgogoro wa wafugaji wa Kakunyu na wawekezaji waliopewa blocks za kufuga katika Ranchi ya Missenyi. Nitashukuru Mheshimiwa Waziri akibainisha alivyotekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mgogoro wa Kakunyu umedumu muda mrefu. Wakati umefika tupate ufumbuzi wa kudumu. Katika kutafuta ufumbuzi wa kudumu itakuwa vyema kuzingatia yafuatayo:-
(i) Vijiji vyote vilivyo ndani Kata ya Kakunyu, Nsunga, Mutukula, Kilimilile na Mabale vilishasajiliwa, vina hati na vinatambulika kisheria;
(ii) Vijiji husika vilikuwepo hata kabla ya Ranchi ya Missenyi na Mabale kuanzishwa;
(iii) Mipaka ya asili kati ya Ranchi ya Missenyi na vijiji inatambulika ni vizuri izingatiwe; na
(iv) Mahitaji ya ardhi ya sasa na vizazi vijavyo lazima yazingatiwe kama alivyoelekeza Mheshimiwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri achukue hatua kwa haraka ili tuweze kupata ufumbuzi wa kudumu. Nashauri pia Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ashirikiane kwa karibu na wa TAMISEMI, Ulinzi na Ardhi ili kupata ufumbuzi wa kudumu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.