Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ELIBARIKI E. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza kabisa na mimi niungane na baadhi ya Wabunge wenzangu kuwapa pongezi Waziri wa Maji, Mzee wangu Mheshimiwa Engineer Kamwelwe pamoja na kaka yangu Mheshimiwa Aweso. Kwa kweli, wanasema mnyonge mnyongeni, watu hawa wanajitahidi kujituma regardless ya changamoto za kifedha ambazo zipo katika Wizara yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nimpongeze Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Mkumbo. Profesa Kitila, kaka yangu huyu kwa kweli, hongera sana brother, tunaona kuna mabadiliko yanaonekana na unatuwakilisha vizuri watu wa Singida pia kwenye Wizara hii, ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na Wabunge wenzangu kuishauri Serikali na hapa naomba tuelewane. Najua Mheshimiwa Waziri wa Fedha yuko hapa, sisi tunapozungumza kama Wabunge tunazungumza kwa niaba ya wananchi walipa kodi wa hii Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wabunge tumesema tunahitaji shilingi 50 ziingizwe kwenye petroli na dizeli kwa ajili ya kuwasaidia wapiga kura wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuishii kuagiza fedha hizi ziingizwe, tunatoa rai fedha hizi zikiingizwa, Wizara ya Fedha tunawataka sisi kama Wabunge, fedha hizi ziende Wizarani zikatatue kero na changamoto ya maji kwa wananchi wetu. Itakuwa ni jambo la aibu kama tutawapa wananchi wa Tanzania burden hii, fedha hizi ziingie zikatumike katika mipango ambayo Bunge hili halikuwa limependekeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi najua Mheshimiwa Waziri wa Maji, najua unyenyekevu wako mzee wangu na Waziri wa Fedha, mama yangu Mheshimiwa Kijaji, wewe ulikuwa mwalimu wangu, huyu mzee mkimpa fedha mimi nina imani kwa jinsi ninavyomjua huyu mzee tatizo na changamoto za maji, mnyonge mnyongeni…

MWENYEKITI: Mu-address kama Mheshimiwa Waziri au Mbunge.

MHE. ELIBARIKI E. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa hiyo, Wizara ya Fedha tunachowaomba hizi shilingi 50 tunaomba ziende Wizara ya Maji wakafanye kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuna watu wengine wanakuja wanachangia kuhusiana na mradi wa Stigler’s. Mimi nataka niwaambie, Ilani ya TANU kipindi cha nyuma, kwa watu mnaosoma historia, acha sisi watu wa Chama cha Mapinduzi, Mradi wa Stiggler’s umekuwepo kwenye Ilani ya TANU enzi za Mwalimu Nyerere, la kwanza. La pili, ndugu zangu tuache kushikiwa akili na Wazungu. Miradi yote ambayo Taifa linajua italeta tija Wazungu wanakuja wanasema environmental problem, achacheni na haya mambo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunachotaka Bwawa la Kidunda lijengwe, mradi huu wa Stiggler’s Gorge ukatekelezwe. Kinachotakiwa Serikali chukueni maamuzi magumu kafanyeni serious land conservation. Kuna mambo yataumiza watu, lakini fanyeni kwa maslahi ya vizazi vinavyokuja na kwa maslahi ya hili Taifa. Haiwezekani leo tuogope kutekeleza mradi kwa sababu tu kuna watu wanapiga kelele kwa maslahi ya Wazungu, tuwaache Wazungu wawili/watatu wakavae bukta wapige picha tuache kutengeneza mradi wa nchi kwa maslahi ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, megawati 2,400 zitaweza ku-curb problem ya umeme ambayo nchi tumekuwa nayo toka uhuru. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri na Serikali, kama Rais wetu alivyosimamia sisi Wabunge wa Chama cha Mapinduzi tunawakilisha watu wengi humu ndani, nendeni mkatekeleze mradi wa Stiggler’s Gorge kwa maslahi ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ukiangalia hata ma-researchers wanavyosema, angalia gharama za uzalishaji umeme kwa kutumia mambo ya thermo technology, angalia mambo ya gesi, angalia mambo ya wave za bahari, angalia mambo ya nuclear, gharama ya uzalishaji umeme kwa njia ya maji ni ndogo, Wazungu wanajua. Hapa tunazungumzia tunajenga treni ya umeme itakwenda kuendeshwa na umeme upi? Kwa hiyo, tuwe wajanja hasa ninyi watu wa Serikali, simamemi imara kuhakikisha kwamba kile mnachoki- dream sisi tunawaunga mkono, tekelezeni kwa maslahi ya wapiga kura wa Jamhuri hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ambalo nataka nilizungumze, Mheshimiwa Waziri nakuomba mzee wangu, kuna Wabunge wamechangia na mimi naunga mkono. Profesa Kitila Mkumbo kaka yangu, unda Tume ukachunguze kuna miradi hapa ya maji imefanyika, mfano mmoja ni kwangu, kuna miradi ya maji imetumia billions of shillings za walipa kodi haifanyi kazi. Nenda pale kwangu kuna Kijiji kinaitwa Nkwairee zaidi ya shilingi milioni 200 zimekwenda, jana nimetoka kufanya mkutano jimboni kwa wapiga kura mradi haufanyi kazi, watu wamepiga pesa, haya mambo hayawezekani. Hatuwezi kuruhusu Taifa letu fedha za walipa kodi zinatumika watu wanakwenda wanafanya miradi ambayo haina tija at the end of the day mradi unakwisha maji hayatoki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga pale kuna mradi ulitekelezwa kutoka Igunga kwenda mpaka kule Isakamaliwa. Nimeondoka nikiwa kama DC pale, DP zote hakuna centre hata moja inatoa maji. Watu wame-relax Wizarani as if nothing has happened, pesa za walipa kodi zimekwenda. Haya mambo kama kweli tunataka kumsaidia Rais na kuwasaidia wapiga kura na kwa maslahi ya chama chetu tuendelee kutawala na kushika dola lazima tutende haki na kuhakikisha kwamba tunawapelekea watu wetu maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la nne, Mheshimiwa Waziri ulikuja jimboni kwangu, nakushukuru sana mzee wangu ukazindua mradi wa maji pale Sepuka na ulituahidi na najua kwa sababu Profesa Kitila Mkumbo uko hapa, Mheshimiwa Waziri alituahidi kutuchimbia visima vingine tisa katika maeneo yafuatayo; Mayaha, Misake, Iseke, Mpetu, Kaugeri, Ufana, Puma na Mpugizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba kwa heshima na taadhima na unajua sasa Profesa Kitila Mkumbo hapa na wewe ni home boy, hebu basi bwana fanya mambo yako huko kwa maslahi ya wananchi na wapiga kura wa Jimbo la Singida Magharibi. (Makofi)

Mheshimiwa Waziri nakuomba utakapokuwa unamaliza majumuisho ya Wizara yako uje na kauli ya kuwahakikishia watu wa Jimbo la Singida Magharibi kwamba kero za maji, kwa mfano, kuna maeneo mzee wangu niliyasema kuna watu wanabeba ndoo za maji kutoka Kata ya Kijiji cha Mlandala…

T A A R I F A . . .

MHE. ELIBARIKI E. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, aah, basi bwana kwa heshima kwa sababu huyu Mbunge pia ninamheshimu basi, lakini kwani hujui kwamba Profesa Kitila Mkumbo ni mwenyeji wa Singida? Nimeipokea taarifa yake kaka yangu huyu, naomba niendelee kumalizia mchango wangu. Natambua kama huyu bwana ni Katibu Mkuu wa nchi nzima lakini wewe kubali tu bwana huyu ni wa kwetu pia Singida kule bwana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumalizia kwa kusema Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Mheshimiwa Dokta John Joseph Pombe Magufuli, mimi nataka nikupongeze sana Mheshimiwa Waziri, toka nimekua kwenye kijiji nilichozaliwa mpaka nimefikisha umri wa kuwa Mbunge sijawahi kuona miradi mikubwa ya maji ikitekelezeka kama kipindi hiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa napozungumza Waziri umeleta fedha shilingi milioni 300 tumechimba maji Mtunduru, shilingi milioni 300 tumechimba maji Irisya, shilingi milioni 81 tumechimba maji Mwaru, shilingi milioni 210 tumesambaza maji Sepuka, shilingi milioni 81 tumesambaza maji Nkwairee japokuwa mradi huu nimesema una matatizo, lakini kwa juhudi kabisa Mheshimiwa Waziri nataka nikupongeze wewe na Naibu wako, ahsanteni sana. Njooni tena tuendelee kutatua changamoto za maji kwenye jimbo langu, Mungu awabariki, endeleeni kuisimamia na kuitekeleza Ilani ya chama changu ili CCM tuendelee kushika dola na tuendelee kuwatumikia wananchi wa hii Jamhuri na walipa kodi wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja asilimia mia kwa mia.