Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuipongeza Wizara kwa taarifa yake ya bajeti. Nitaongea machache tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kuhusu walimu wastaafu. Kuna walimu waliostaafu toka mwaka 2016 lakini mpaka leo bado hawajalipwa posho ya nauli ya kuwarudisha makwao. Serikali inatuambia nini kuhusu wastaafu hawa ambao hawajui hatma ya posho yao ya nauli ya kuwarudisha makwao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni UMISHUMTA. Shule za msingi zinashiriki michezo hiyo. Je, Serikali inatuambia nini kuhusu shule kuwezeshwa fedha kwa ajili ya kuwahudumia wanafunzi wakati wanashiriki michezo? Kuna baadhi ya wanafunzi wanatoka mbali kwenda kushiriki michezo na wakati huo wengine wanatoka majumbani kwao ikiwa hawajakula chochote? Je, Serikali haioni ushiriki wa wanafunzi hao wao katika michezo mbalimbali utadhoofika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu madai ya walimu. Kuna baadhi ya Halmashauri zinadaiwa fedha na walimu zikiwemo za likizo na kusimamia mitihani ya darasa la nne na la saba. Tunaomba Serikali ifuatilie Halmashauri huenda kuna baadhi ya Halmashauri zinafanyia ubadhirifu maslahi ya walimu. Hii pia inachangia kushuka kwa morali ya walimu kufundisha madarasani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu jengo la Kitega Uchumi la CWT lililopo Ilala Boma, Dar es Salaam. Chama cha Walimu kilichangisha walimu sehemu mbalimbali kwa ujenzi wa jengo hilo. Kuna walimu waliostaafu au kufa ambao walichangia fedha zao. Je, Serikali itueleze, walimu wananufaika vipi na kitega uchumi hicho? Je, wale waliostaafu au kufa watanufaikaje?