Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee kuhusu michango iliyokithiri kwa shule za private. Shule za msingi na sekondari za private wanatozwa michango mingi mno. Shule za private za msingi zinatozwa shilingi 1,000 kila mtoto kwa ajili ya ukaguzi wa shule; shilingi 1,000 kila mtoto kwa ajili ya michezo; shilingi 3,500 kwa kila mtihani wa mock wa kila mtoto; shilingi 15,000 kila mtoto kwa mitihani ya kitaifa. Hata shule zinazosaidia watoto nao wanatozwa michango hiyo. Naiomba Serikali ipunguze utitiri huu wa michango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kukariri masomo. Watoto wengi wanaokwenda kusoma kwenye shule za private wanabadilika na kuwa na matokeo mazuri kutokana na utaratibu wa kukariri. Hivyo watoto wengi wanakazana
kusoma kwa sababu wanaogopa wasiposoma kwa bidii watarudia. Hivyo wanakazana sana. Naiomba Serikali irudishe utaratibu wa kukariri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watoto ambao wana vigezo vya kupata mikopo lakini hawapati mikopo hiyo. Naiomba Serikali iangalie wanafunzi wenye vigezo wapewe mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na mmomonyoko wa maadili katika nchi yetu, naiomba Serikali kuingiza kwenye mitaala suala zima la maadili. Kwa kuwa wanafunzi wa kike wanapata ujauzito kutokana na kuishi mbali na makazi yao, lakini pia wanafunzi wengi wa kike wanapanga mitaani, naiomba Serikali ihakikishe inaongeza hosteli kwa ajili ya watoto wetu wa kike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali iingize masomo ya ujasiriamali kwenye mitaala ili baadae watoto wetu wajue namna ya kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.