Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. BALOZI ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga mkono na kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri mnayoifanya. Nachangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu ambao umefanywa wa kugawa vifaa vya maabara katika shule za sekondari unapaswa kupongezwa sana, ila katika mgao uliopita Wilaya ya Muheza tulipata mgao wa shule saba tu. Naomba kwenye mgao huu Muheza tuongezwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Muheza hatuna Chuo cha VETA. Naomba tuone uwezekano wa kujenga. Kipo Chuo kimoja maeneo ya Kiwanda Potwe ambacho kipo chini ya Ustawi wa Jamii. Chuo hiki hakifanyi vizuri na uongozi wa Wilaya utaomba kifanywe VETA. Ombi hilo likifika naomba lishughulikiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliwahi kuleta ombi la Muheza High School iweze kuangaliwa na iruhusiwe kuwachukua wanafunzi wa kutwa. Hii itasaidia wanafunzi waliofaulu na kukosa nafasi, maana shule hiyo imejengwa kwa nguvu za wananchi.