Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SEIF K. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kupongeza juhudi zinazofanywa na Wizara yako katika kuboresha hali ya elimu Tanzania. Tumeshuhudia sehemu mbalimbali za nchi madarasa, madawati, mabweni katika shule za msingi, shule za sekondari na hata vyuo. Hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu sera ya nchi juu ya kila Wilaya kuwa na VETA. Nipende kurudia tena katika Wilaya ya Igunga, Kata ya Choma Chankole tulipata ufadhili wa ujenzi wa madarasa manne kutoka ufadhili wa NGO ya World Vision IDP Manonga.

Tunawashukuru sana na tayari wameshakabidhi katika Halmashauri. Sababu ya kutokuwa na fedha za kutosha, tunaomba sasa Wizara itusaidie ujenzi wa ofisi na mabweni ili chuo hiki kianze kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ukitupatia shilingi milioni 400, tunao uwezo wa kuboresha zaidi VETA hii kuwa ya kisasa. Naomba sasa Wizara ipokee ombi hili kwa mara nyingine tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja ya kupitisha bajeti yako.