Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kushukuru kwa nafasi hii. Nampongeza Mheshimiwa Waziri Profesa Ndalichako kwa hotuba nzuri na yenye kuleta matumaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Mafia kwa kushirikiana na Mbunge wao wamefanikisha kujenga Chuo cha Ufundi, VETA. Majengo na miundombinu ya chuo hicho yameshakamilika na wanafunzi wameshaandikishwa na wameanza masomo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto tuliyonayo sasa ni usajili wa chuo. Tumeshafanya taratibu zote na Wakaguzi wa Kanda, wamekuja Mafia na kukikagua chuo na wameonesha kuridhika kwao na majengo, miundombinu na wana taaluma na wakufunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaiomba Wizara itusaidie kuharakisha usajili huu kwani Mafia ni miongoni mwa maeneo ya pembezoni na kuwavusha wananchi waje Dar es Salaam. Ni changamoto kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la shule binafsi kudahili wanafunzi na kisha kuwachekecha kwa mtihani migumu ili kupata wanafunzi best na kupata viwango bora, ni jambo ambalo Wizara lazima ilitupie macho, kwani linawanyima haki vijana wetu kwa uroho wa wamiliki wa shule ili kupata viwango bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninaunga mkono hoja.