Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi naomba kuchangia hotuba ya bajeti hii ya Elimu, Sayansi na Teknolojia; binafsi nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Joyce Ndalichako, dada yangu kwa kumudu Wizara hii na sote tunaona namna anavyochapa kazi. Namuombea asirudi nyuma, azidi kusonga mbele ili kuhakikisha anatatua changamoto za elimu, ukosefu wa nyumba za walimu, ukosefu wa vyoo, ukosefu wa madarasa, ukosefu wa maabara na vifa vya kufundishia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi nijielekeze kwenye changamoto mbalimbali zinazoikabili Halmashauri yetu ya Uvinza.

Mhesimiwa Mwenyekiti, moja; tunazo shule ambazo zinajengwa na wananchi na kumaliziwa na Halmashauri na pia Mfuko wa Jimbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano shule ya sekondari Mwakizego; shule hii imepokea hadi walimu wa Serikali na ina jumla ya madarasa kumi. Imejengwa ili kupunguza umbali wa watoto wetu kutembea hadi Ilagala sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe dada yetu Mheshimiwa Joyce Ndalichako mambo mawili; kwanza, kuisajili shule hii kabla ya mwaka wa bajeti tarehe 30 Juni, 2018. Pili, nimuombe aje atembelee shule hii ili aone jitihada za wananchi wa Mwakizega.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walimu hawa wapya inakaribia miaka miwili hawalipwi pesa zao za uhamisho hadi leo. Sambamba na hili walimu wengi wana malalamiko ya kutolipwa pesa zao za stahiki zao mbalimbali ikiwemo na kucheleweshewa kupandishwa vyeo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu shule mbili za Lugofu Girls High School na Lugofu Boys; shule hizi ziko kwenye majengo yaliyoachwa na UN (Kambi ya Wakimbizi).

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule hizi pia Serikali imezisahau, kwa nini wasipewe pesa kwa ajili ya kujenga mabweni mazuri ya kisasa na vyoo? Kwa nini vyoo wanavyotumia haviko kwenye hali nzuri kabisa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo shule za msingi nyingi ziko kwenye hali mbaya sana, tunayo shule ya msingi Anzerani ina madarasa mawili zaidi ya miaka minane na nyumba ya walimu two in one, imepaliliwa lakini hakuna pesa za kuimalizia.

Tunaomba Wizara itupatie upendeleo wa fedha za ujenzi wa madarasa ili tuweze kujenga madarasa kwenye shule zote zenye uhaba wa madarasa. Kwa mfano shule ya msingi Msimba ina darasa moja kwa zaidi ya miaka 10. Sambamba na haya tunao uhaba mkubwa wa walimu wa shule za msingi, hali ya miundo mbinu ni mbaya, vyoo na nyumba za walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Uvinza hatuna Chuo cha VETA na wanafunzi wanaomaliza shule ya msingi na sekondari wengi hawapati ufaulu wa kuendelea na shule za sekondari na high school; kwa nini Serikali isianzishe Chuo cha VETA Ilagala ili kunusuru vijana hawa?