Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichangie kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya na uzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri inayofanya hasa katika sekta hii ya elimu, sayansi na teknolojia. Nampongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa maamuzi yake ya kutoa elimu ya msingi bure. Watanzania wengi hasa wenye kipato cha chini watapata haki ya elimu.

Mheshimwa Mwenyekiti, naomba nishauri katika maeneo machache; moja, nashauri Serikali iangalie namna ya kurejesha asilimia mbili iliyochukuliwa mwaka 2014 kutoka Skills Development Levy ya asilimia nne kwenda kwenye Bodi ya Mikopo kwa ajili ya dharura. Kwa sasa urejeshwaji wa mikopo hiyo ni nzuri basi asilimia mbili irudi kwenda kwa skills development (VETA).

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya vyuo vyetu vya ufundi (VETA) ni mbaya sana na tunahitaji mageuzi makubwa. Leo hii kila kitu ni kutumia teknolojia ya computer (IT). Kwa mfumo wetu wa sasa wa VETA tunatumia mfumo wa miaka ya nyuma ambapo hazifundishi kutumia IT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ufundi kwa mfano wa magari (umeme) yote inategemea mfumo wa IT wa kutumia diagnostic equipment. Umeme wa majumbani pia vyombo na vifaa vyenye (sensors) kutumia programu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawahitimu wengi wa vyuo vikuu (shahada)/wenye digrii. Kwa sera ya viwanda tunahitaji kuwa na mafundi (technician). VETA kwa mfumo wa kisasa unaweza kuwa mkombozi wa ajira kwa Watanzania. Mfumo wa elimu wa apprentice utasaidia Watanzania mbalimbali wenye ujuzi wa ufundi kupata elimu rasmi na kujiboresha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashukuru Wizara kutukubalia VETA Manyara kupata mradi wa Wajerumani wa mafunzo ya apprentice. Tunashukuru pia kwa kutuweka katika bajeti ya kukarabati na kuongeza karakana ya Babati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri pia mnapogawa fedha za miradi ya kukarabati mgawe kwa uwiano kwa kufuata idadi za shule katika Halmashauri na idadi ya watoto na mazingira. Sisi Halmashauri ya Babati tumepata shule moja tu, shilingi 60,000,000; Halmashauri yenye shule mbili kati ya 137. Wilaya zenye shule 30 zimepata shule mbili zaidi ya shilingi 170,000,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri COSTECH ipatiwe vyanzo vya kudumu ili angalau ipate shilingi bilioni 100 kwa mwaka. Hali ya utafiti nchini ni mbaya na sehemu kubwa inategemea ufadhili wa nje kwa kuendesha tafiti zao; tukumbuke mfadhili hutoa anapokuwa na maslahi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine kirudishwe chini ya Wizara ya Kilimo na Umwagiliaji kwa usimamizi, wataweza kukitendea haki kwa kufuatilia kwa karibu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itoe unafuu wa kodi ya mapato kwa mashirika na wadau kwenye michango yao ya kwenye sekta ya elimu au huduma za jamii.