Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia katika Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na suala la upungufu wa walimu wa shule za msingi; hakuna elimu bila walimu, elimu bure bila walimu haitasaidia kama hakutakuwa na idadi ya kutosha ya walimu wenye weledi na motisha ya kufanya kazi ya kufundisha. Ningependa kujua Serikali imeajiri walimu wangapi mpaka sasa ili kukabiliana na upungufu huo? Serikali ina mkakati gani endelevu wa kuhakikisha tatizo la upungufu wa walimu linatoweka kabisa? Serikali imepanga kuajiri walimu wangapi katika mwaka wa fedha 2018/2019?

Mheshimiwa mwenyekiti, niongelee tatizo la uhaba wa vitabu katika shule zetu za msingi, unakuta kitabu kimoja kinasomwa na watoto watano mpaka sita, hii inaleta usumbufu mkubwa kwa watoto wetu na uelewa kuwa mdogo. Je, ni lini Serikali itahakikisha tatizo hili la upatikanaji wa vitabu linakwisha katika shule zetu? Mbali na upatikanaji mdogo wa vitabu bado vitabu hivyo vina mapungufu makubwa ndani na tatizo hili limekuwa likijirudiarudia pamoja na Wabunge kulisemea humu ndani. Je, tatizo ni nini? Ni akina nani wanafanya uhakiki huo wa vitabu? Kwa sasa hivi tunategemea nini kwenye uelewa wa watoto wetu? Itakuwaje kama vitabu vina makosa kwa watoto wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya mwaka juzi nilimuomba Mheshimiwa Waziri kulifanyia kazi kwa haraka suala la wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi waweze kupelekwa kwenye shule za sekondari za wanafunzi walio na ulemavu, lakini hilo halikufanyika. Wanafunzi hawa wamechanganywa na wanafunzi wasio na ulemavu, hii hatuwatendei haki watoto hawa. Kwa mfano shule ya watoto wenye ulemavu Njia Panda darasa lilikuwa na watoto 20 na wote wamefaulu, nimpongeze mwalimu mkuu na walimu wote wa shule hiyo kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa watoto hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu hapa ni kwamba kwa sababu uelewa wao ni wa taratibu, hivyo wanatakiwa kuwa na walimu wanaowafundisha na kuwafuatilia kwa karibu. Si kwamba watoto hawa hawana akili ila wanahitaji ufuatiliaji. Hawa watoto kumi waliofaulu wamepelekwa shule ya ufundi Moshi wanane na wanafunzi wawili wamepelekwa shule ya sekondari Mbulu. Niombe kujua, Serikali ina mpango gani na watoto hawa? Ni lini shule za sekondari za watoto wenye ulemavu zitajengwa za kutosha ili watoto wetu wapelekwe huko ambapo watapata walimu na vifaa kwa ajili ya aina ya ulemavu walio nao? Tusipofanya hivyo watoto hawa watafeli wengi na maisha yao hayatakuwa na mwisho mwema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.