Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa taarifa ya awali kabisa kuwa naunga mkono hoja hii ya Mhesahimiwa Profesa Joyce Lazaro Ndalichako (Mb) Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa asilimia mia moja. Aidha, nichukue fursa hii kumshukuru Mheshimiwa William Ole Nasha (Mb) Naibu Waziri wake kwa kazi nzuri anayoifanya ya kumsaidia Waziri wake kwa uaminifu na uadilifu mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika Profesa Ndalichako amethubutu kutembelea Wilaya ya Namtumbo na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Chuo cha VETA kinachojengwa katika eneo la Suluti, Wilaya ya Namtumbo. Niombe radhi kwa niaba ya wananchi wa Namtumbo waliojipanga kumpokea lakini walichelewa kuja au tuseme kwa fikra za wananchi hao Mheshimwa Waziri aliwahi sana kuingia Wilayani humo, akizingatia kauli mbiu ya kipenzi cha wana Namtumbo Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wetu ya “Hapa Kazi Tuu!

Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako (Mb) wananchi wangu watafurahi sana kama utawapa fursa ya kukukaribisha kama mkombozi wao kwa kuwazawadia mambo makubwa yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni ujenzi wa Chuo cha VETA katika Wilaya na hivyo mafunzo yatakapoanza kutolewa tutapata fursa ya kushiriki katika uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili utoaji wa fedha (milioni 180) zilizowezesha kujenga majengo ya kisasa ya shule ya msingi mpya katika Kitongoji cha Miembeni/Chatisa na Kijiji cha Likuyu Mandela na hivyo kuondoa jengo hafifu lililoezekwa kwa nyasi lililokuwa likitumika kwa watoto wa darasa la kwanza hadi tatu na kama sehemu ya shule ya Likuyu Mandela walitenganishwa na Mto Usio na daraja la uhakika na lisilopitika kipindi cha masika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, kukipokea Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Mputa na kuwawezesha wanafunzi kufanya mitihani yao chini ya mitaala ya VETA. Mheshimiwa Waziri , chuo hiki kina changamoto lukuki ambazo zinahitaji kushughulikiwa na Wizara yako.

Mhesimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri licha ya kuzikabili changamoto za Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Mputa, utusaidie kuweka msukumo wa hali ya juu kwa majengo ya Chuo cha VETA cha Namtumbo yakamilike kujengwa kwa wakati kwa awamu zote mbili ikiwa ni pamoja na kujengwa mabweni ya wanachuo na kantini ili mafunzo yaanze kabla ya mwaka 2020.

Mheshimiwa Waziri, tunacho Chuo cha Ualimu cha Nahoro kinachomilikiwa na Chama Kikuu cha Ushirika cha Songea na Namtumbo (SONAMCU). Nimehakikisha mfuko wa jimbo (CDCF) unachanga katika kutekeleza masharti ya kukiwezesha kiendelee kutoa mafunzo ya ualimu ngazi ya astashahada.

Aidha, mmetufungulia shule nne za kata kati ya 23 tulizonazo kutoa elimu ya kidato cha tano na sita. Nguvu za wananchi zimechangia katika kujenga majengo mapya yaliyohitajika katika kuziwezesha shule hizo za sekondari za Kata za Nanungu, Luegu pamoja na Namabengo kuweza kutoa elimu ya kidato cha kwanza hadi cha sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri atusaidie kuboresha utoaji wa elimu katika shule hizo hususan majengo, walimu na vitabu.