Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni mwendelezo wa mchango wangu wa maongezi. Tofauti na juhudi ndogo inayowekezwa na Serikali katika kumuandaa kijana kuweza kujiajiri nje ya mfumo wa ikama ya Serikali, pia Serikali imeshindwa kusimamia sekta binafsi hususani financial institutions ili kuweza kutoa ajira za kutosha kwa vijana wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TBL leo ime-downsize waajiriwa wake kinyume kabisa na matakwa ya sera ya ajira. TBL amehamishia payroll Mauritius kwa kuwa kwa kuhamishia payroll nchi ya Mauritius definitely mwekezaji anaingia tax heaven na kwa kufanya hivyo kumenyima vijana wetu ajira.

TBL imebaki na gate keepers na Idara ya Uzalishaji. Tanzania imebaki kuwa na idadi kubwa ya walevi ikiashiria pengine ndiyo sehemu ya faida ambayo nchi imejipanga kupokea kupitia uwekezaji wa TBL. Swali langu ikiwa hivi ndivyo, nini hatma ya Mfuko wa Bodi ya Elimu ya Juu? Vijana hawaingii kwenye soko jipya la ajira na walioko kwenye soko la ajira wanatolewa nje pasipo kauli yoyote ya Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia taasisi za fedha (banking industry) it almost kama haipo. Benki za Standard, NBC, Stanbic pamoja na Barclays kazi ya IT yote inafanyika Kenya, ukija sehemu ya malipo kazi hizi zinafanyika nchi ya Chennai - India na servers za IT zikiwa hosted nchi ya South Africa. Personally nimewahi kumfuata Waziri wa Mipango kwenye kikao cha Bunge la Bajeti mwaka 2017/2018 na alichonieleza ilikuwa hii ni common practice kwa nchi za Afrika na hata Ulaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Elimu inazalisha vijana wa kutosha fani ya IT - DIT na UDSM- Engineering Department na kwenye baadhi ya taasisi za elimu ya juu, lakini kwa utamaduni huu hatuwezi kufikia malengo ya urejeshwaji makini kwa Bodi ya Mikopo. Aidha, wakati Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mpango akinijibu hoja hii ambayo nilimfikishia mezani kwake na akanijibu kuwa hii ni common practice amesahau nchi za Uganda na Mozambique wanafanya vizuri kabisa kazi za IT katika sekta za mabenki ziko hubbed nchini mwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, rai yangu kwa Serikali ni vema Wizara ya Elimu ikafanyia kazi hoja za CAG juu ya wasiwasi wake na uhimili wa Mfuko wa Bodi ya Mikopo. Ikiwa Mashirika ya uwekezaji yataachiwa yajiendeshe holela kwa kufuta ajira za vijana wetu hii itapelekea:-

(i) Kuchochea kasi ya ukosefu wa ajira kwa nchi yetu;

(ii) Ku-drain skills, capability and knowledge za vijana wetu wa fani ya IT kwa kuendelea ku-outsource kazi nyingi nje ya nchi kwani mwisho wa siku hata Serikali ni vigumu sana ku-realize dividend na kupoteza fedha nyingi na hata kuondosha ari ya kuzalisha ajira kwa vijana wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho Serikali ione namna bora ya ku-motivate walimu elimu ya juu. Madai ya walimu elimu ya juu hayafanyiwi kazi, walimu wamesimamishwa promotions kinyume kabisa na matakwa ya miundo ya utumishi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, I submit, naunga mkono hoja.