Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu zoezi la kuhamisha walimu kutoka sekondari kwenda kufundisha shule za msingi; zoezi hili limewakatisha tamaa walimu kwa kuwaharibia malengo yao. Wapo walimu ambao walikuwa na malengo ya kufundisha sekondari na kuendelea kusoma zaidi ili wafundishe Vyuo vya Ualimu, hata Chuo Kikuu. Unapomrudisha mtu ambae alikuwa analenga huko ukampeleka kufundisha shule ya msingi unaharibu malengo yake kitu ambacho ni kibaya na ninaamini hamuwezi kuwafanyia watoto wenu hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, maandalizi ya zoezi hili hayakuwepo ni kwa nini Serikali haikutangaza ili wale wanaopenda kurudi kufundisha primary wajitokeze kwa hiari yao (naamini wapo) na wale wasiopenda wabaki. Ni hakika wapo walimu ambao wamebaki kufundisha sekondari bila kupenda kukaa huko. Hii ingetoa nafasi mtu kwenda kwa utashi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, zoezi hili limegubikwa na fitna, ukabila, siasa na rushwa pale ambapo Afisa Elimu na Mwalimu Mkuu hawapatani na mwalimu fulani anampeleka primary kama adhabu.

Mheshimiwa Mweneykiti, napenda pia kuongelea taratibu za uteuzi wa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba kwenda sekondari hasa shule za kata. Katika uteuzi huu umbali hauzingatiwi, watoto wanatolewa kwenye shule za karibu na kuwapeleka mbali na nyumbani umbali wa kilometa saba hadi 10 kwenda na kurudi. Wazazi wanashindwa kutoa nauli kwa watoto wao. Naomba umbali uzingatiwe hasa kwa watoto wa kike ambao wanapewa mimba na bodaboda wanaowasafirisha kwenda mashuleni.