Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishauri Serikali kuwa watoto wasio na uelewa wa haraka kukaririshwa hakuepukiki kwa ajili ya ustawi wa Taifa letu. Ni ukweli usiopingika kuwa wapo ambao wanaingia kidato cha kwanza kupitia maswali ya kuchagua ambayo hata mwanafunzi akifumba macho ana uwezo wa kupasi. Katika hili, naomba tufike mahali tubadili mtindo wa maswali tuwe na mtindo wa kupima uelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili niongelee kuhusu motisha kwa walimu. Naishauri Serikali kuwatia moyo walimu badala ya kuwavunja moyo kwani wanafanya kazi katika mazingira magumu. Inapotokea kupewa majibu yasiyostahili kutoka kwa viongozi wa Serikali au mfano Wakuu wa Wilaya kuwapa adhabu, hekima ingeweza kutumika kutatua matatizo yanayojitokeza. Nashauri Serikali kuweka mazingira rafiki ya kufundishia mfano walimu kuwa na nyumba karibu na mahali wanapofundisha. Niishauri Serikali kuhakikisha inaongeza fedha kwenye eneo la vifaa vya kufundishia mfano karatasi za kutungia mitihani ili kutoa mitihani ya mwezi kiurahisi kwa ajili ya kupima maendeleo ya wanafunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, napenda kuongelea kuhusu ukaguzi. Niishauri Serikali kujipanga kwa ajili ya kuhakikisha vifaa vinakuwepo kama magari ya kuwapeleka wakaguzi kwenye shule mbalimbali kwa ajili ya kufanya ukaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, niishauri Serikali kuwekeza katika kumkomboa mtoto wa kike kwa kuwajengea mabweni ili kuwaondoa katika shida hii ya kupata ujauzito wakiwa shuleni. Watoto wa kike wameshindwa kufikia malengo yao ya baadae kutokana na mazingira yasiyo rafiki katika kujifunzia, mfano umbali mrefu na mapori kwa ajili ya kuzifikia shule hizo hivyo humo njiani kukutana na majanga ya kubakwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tano ni ucheleweshaji wa fedha. Serikali inachelewesha fedha hivyo mipango mingi kushindwa kutekelezeka kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sita, nishauri juu ya chakula shuleni. Mpango wa chakula shuleni unasaidia wanafunzi kuwa na utulivu na kujifunza kwa urahisi. Niishauri Serikali kuweka utaratibu mzuri wa kuwepo chakula shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, saba ni uhaba wa walimu. Niishauri Serikali kuliangalia hili kwani mwalimu kufundisha watoto mia moja darasa moja na ana vipindi vinne kwa siku na hivyo kuwa na madaftari 400 ya kusahihisha kitu ambacho hawezi mwalimu kufanya kwa usahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, niishauri Serikali kuweka utaratibu wa kukariri ili kuboresha elimu ya Tanzania.