Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Wizara kwa kazi kubwa inayofanya kuboresha elimu kwa Watanzania. Mimi nizungumzie suala la vitabu kwa mtaala mpya kwa shule za msingi. Baada ya mtaala huu kusambazwa shuleni walimu walipewa mafunzo juu ya mtaala mpya lakini vitabu vinavyofaa kwa mtaala huo vimechelewa kufika. Hii inawapa kazi ngumu sana walimu hasa wa darasa la kwanza mpaka la nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Jimbo langu na Wilaya nzima ya Itilima vitabu hakuna kabisa. Kwa hiyo, tuna mtaala mpya lakini vitabu havipo. Naiomba Serikali iharakishe kuleta vitabu ili walimu waone unafuu wa kufundisha watoto wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naunga mkono hoja.