Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kupata nafasi ya kuchangia katika eneo hili muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze hapa ambapo mwenzangu ameishia. Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu sana juu ya ama kutungia kiingerea au kiswahili. Hili ni jambo ambalo kwa kweli Mheshimiwa Waziri, Profesa inatakiwa Serikali ilitolee maamuzi mapema kwa sababu kadri tunavyovuta muda maana yake tunazidi kuchelewa kufanya maamuzi ya mambo yetu na kuweza kuboresha elimu yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nadhani hili ni jambo la muhimu sana kwa sababu wamelifanyia kazi, tafiti zimefanyika, wataalam wameandika na Profesa anajua. Kwa hiyo si jambo la kuvutana tena, aje atueleze nini msimamo wa Serikali, tunafanyaje? Tunaamua kutumia kiingereza kufundisha kutoka chekechea mpaka Chuo Kikuu au tunaamua kutumia kiswahili? Tuamue ili tusiwe na double standard katika elimu yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningeomba Mheshimiwa Waziri atusaidie, nimesoma bajeti yake ambayo ameleta kwenye Bunge hili tukufu ili tuijadili, na bahati nzuri huyu ni mwalimu. Lakini jana wafanyakazi wa nchi hii popote walipokuwa, hata wagonjwa waliamka vitandani wakakaa wakitazama kumsikiliza Mheshimiwa Rais kwamba angalau kwa sababu aliwaahidi kwamba ataongeza mishahara angeweza kusema neno jana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa bahati mbaya sana ameeleza mipango mingi ya Serikali, lakini hakusema ataongeza mishahara kwa watumishi lini na hasa walimu ambao wamekuwa na malalamiko kwa muda mrefu sana. Hili ni jambo ambalo kwa kweli na ile speech ya Rais Mheshimiwa Magufuli Rais wetu wa Tanzania na Rais wa Kenya ziliwekwa pamoja parallel, kwa hiyo, wakawa wanalinganisha kwamba Uhuru Kenyatta yeye ameongeza asilimia tano, lakini sisi tunasema tunaangalia kwanza, tunatoa ahadi mpaka leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu sana kumbukumbu ziwe sawa. Rais aliwaahidi wafanyakazi ataongeza mshahara mwaka jana mwezi wa tano, sasa mwaka huu tena ameenda kuahidi kwa hiyo nadhani mumsahauri vizuri, kama jambo haliwezekani, hilo jambo lisitamkwe, watu wanakuwa na matumaini hewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ina shida kubwa sana ambazo Mheshimiwa Waziri alipaswa atueleze kwenye bajeti hii. Kwa mfano, kumbukumbu zinaonesha kwamba tuna shida mpaka ya matundu ya vyoo katika nchi hii. Kwa mfano shule ya msingi peke yake kuna upungufu wa matundu ya vyoo 239,716, kwenye bajeti ya waziri anaonesha kwamba watajenga matundu ya vyoo ambayo ni asilimia 0.73 ndiyo yatakayojengwa kwa mwaka huu wa fedha. Sasa nimejaribu kupunguza hapa hayo ni matundu 2,000 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 lakini ukipunguza hapa kwa matundu 239,000 maana yake tuna upungufu wa matundu ya vyoo 235,000 bado unaweza ukaona shida ni kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la madarasa, kwenye bajeti anaonesha kwamba mwaka huu atajengwa madarasa 2,000, lakini shule za msingi peke yake tuna upungufu wa madarasa 107,000 ukipunguza maana yake tunadaiwa madarasa 107,000. Nyumba za walimu, upungufu uliopo unaonesha shule za misingi 178,435, sekondari 69,816 lakini Mheshimiwa Waziri anasema watajenga nyumba 56. Ukitafuta asilimia ni 0.023, ndiyo asilimia itakayojengwa. Kwa hiyo ningedhani kwamba malalamiko ya wananchi na walimu na wadau ni kwamba inatakiwa tuoneshe hizi kero zilizopo tunapunguza kwa kiwnago gani? Kama unapunguza asilimia 0.02 kwa kweli sio sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine masomo; kwa maana ya upungufu kwa somo. Kama unaambiwa tuna nchi ya viwanda, halafu walimu wa hesabu tuna upungufu wa walimu 7,291, biolojia ni walimu 5,181, kemia 5,377, fizikia ni 6,875; na hapa nichukulie kwa mfano Mkoa wa Dar es Saalam kuna labaratory technicians pale mahitaji ni 67 tulikuwa nao mwaka jana saba tu peke yake maana yake hao walimu pamoja na madai yao na mapungufu, changamoto mbalimbali wanafanya kazi ya kufundisha mara mbili na hakuna malipo ya ziada. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo limechagizwa na Serikali, kuhusu elimu ya bure, na mimi nimekuwa nikipinga mara zote kwamba Tanzania hakuna elimu ya bure, kuna elimu imepunguzwa gharama zake. Serikali ilichofanya imeondoa ada, lakini mambo mengine yatabaki na tukubaliane haiwezekani Taifa hili kila kitu kikatolewa bure bure, watu wote watakuwa wazembe, itakuwa ni ulemavu. Kuna wajibu wa wanafunzi wenyewe wafanye mitihani wafaulu, kuna wajibu wa wazazi na walezi wasimamie na kuna kazi za kufanya, kuna wajibu wa walimu wafanye kazoo yao na kuna wajibu wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini haiwezekani leo kwa mfano shule haina maji wale wazazi wangekaa vizuri pamoja wakajadiliana, wanaweza wakachimba visima shuleni na maji yakaondoka. Kuna upungufu wa madarasa, wangeweza kuchangisha, darasa moja wangechanga bilioni 21, una shule ina wanafunzi 2,000 wale wazazi ambao hawana uwezo wangewekwa pembeni, wale wazazi wenye uwezo wakubaliane, jambo hili linawezekana.

Kwa hiyo, mnapowaaminisha wananchi kwamba elimu ni ya bure watu wanabweteka, inawezekanaje watu wawazae watoto wao, wawapeleke shuleni, wakae miaka minne wasichangie gharama hawawajibiki, hili taifa litakuwa Taifa la wazembe kweli kweli. Huu uzembe, ni ugonjwa ambao unalelewa ambao hatuungi mkono. Kuna watu ambao wanapaswa kusaidiwa na kuna watu ambao wanaweza kufanya kazi hiyo na michango ni ya hiari, wale ambao wanaweza wafanye kazi hiyo, hili jambo si sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utafiti unaonesha asilimia 60 au zaidi ya wanafunzi ambao wanamaliza form four hawa wanapata divison zero, divison four, Wabunge na wananchi wanauliza, hawa watoto baada ya kupata zero na for wanaenda wapi? Ndiyo maana inakuja hoja hapa ya VETA, na mnataka watoto wapate mimba katika umri mdogo. Sasa mtoto anamaliza darasa la saba hakwenda sekondari au kaenda kapata zero, hana ufundi wowote hata kufika hawezi kupika, hata bustani hawezi kulima, hivi vyuo vya ufundi ni muhimu sana. Mheshimiwa Ndalichako haya ndiyo majibu unatakiwa uje hapa utuoneshe, mkakati ukoje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu, shule za sekondari na shule binafsi. Mimi ni mwalimu na nimefanya utafiti mdogo. Shule yangu moja, ni-declare (to declare) ilikuwa ya mwisho lkatika shule za Tanzani form four mwaka jana, inaitwa Nyebulu Sekondari. Nimeenda shuleni pale walimu wanasema na mnawazuia private wasigawanye, lakini kuna shule za vipaji maalum, maana yake tayari huu ni ubaguzi, wamelekwa pale wenye uwezo mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna shule za mikoa wamepelekwa, kuna shule za kata, hizi za kata ndizo class c. Mheshimiwa Ndalichako, kwanza mmetunga maswali ya kuchagua mpaka hesabu na mnataka nchi ya viwanda na nilipowauliza mkasema hapa ni muda, suala sio muda! Kama mtu hana uwezo wa kwenda high school, asiende, lakini akibaki mahali uwepo mpango mkakati wa kumsaidia apate uwezo wake wa kuishi. Msipeleke watoto shuleni kisiasa, wazazi wanaamini wameenda shule kumbe kimsingi wamelekwa, unapata asilimia ndogo unaenda sekondari. Miaka minne unakula ugali wa baba na mama, shambani huendi, huchangii Pato la Taifa, unapata zero. Huyu mtoto atajengewa chuki kwenye jamii yake, watu wanatakiwa wajue, kama huna uwezo wa kwenda sekondari usiende ufanye kitu kingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Profesa, unatungaje maswali ya kuchagua ya hesau halafu taifa liendelee? Unatungaje kazi hiyo? Halafu mnachokifanya katika mfumo wa maswali ya mtihani ana ana ana doo, watoto waansinzia, anaangukia hapa nda! Halafu ninyi mmechukua wanafunzi ambao hawana uwezo kwenye shule za kata mmerundika kwenye darasa moja yaani asie na uwezo amekaa na asie na uwezo mwenzake, nani anamuuliza mwenzake swali? Hii ni changamoto, halafu mnataka kutuletea hapa.