Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa na mimi kuchangia mada iliyopo hewani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uhaba wa muda nitaenda moja kwa moja na ajenda yangu. Awali ya yote nitapenda kuzungumzia ufaulu mbaya kabisa wa wanafunzi wa form four. Mwenzangu ameenda Chuo Kikuu moja kwa moja huko kwenye masters, mimi nitakuja hapa kwenye vijana wetu hawa wa form four.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukijigamba sana Watanzania kwamba tunafanya vizuri sijui tuko vizuri, tumepata sijui wanafunzi hamna, sana sana tuko below 30 percent ya wanafunzi wote wanaofanya mitihani. Kwa wakati huu na kwa ukubwa wa nchi hii na kwa wataalam tulionao ndani ya nchi hii, hii ni aibu, kwamba tunafanya mitihani ya Taifa wanaofaulu below 30 percent nchi nzima ni aibu, sana ni private schools ndiyo zinajikakamua kidogo, lakini hizi za kwetu hizi I mean government school hamna kitu. Ukiangalia matokeo acha shule hizi za vijijini ukiachia labda hizi za mijini kama Dar es Salaam, Arusha, Mwanza pengine na Zanzibar pale mjini, huko vijijini “F” zinatafunana pale. Unaweza ukafikiria labda…

T A A R I F A . . .

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba uniachie tu niendelee nimuachie na hayo yake kwa sababu tunajua kwamba wajenga shule ni sisi Watanzania, lakini hiyo ni lugha ya kiswahili na yeye ni mswahili anafahamu hiyo lugha maana yake nini. Kwa hiyo, naomba unilindie muda wangu niendelee na kuchangia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani tungeangalia hapa form four kuna tatizo gani hapa, shule zinazofanya vizuri zaidi ni za private, narejea tena hizi za kwetu bado. Kwa hiyo, kwanza tungeangalia yawezekana kuna matatizo kidogo kwa walimu wetu hawa, yawezekana there are some of the topics zinawasumbua, ni vema tungefanya research tukatumia ile Idara ya Ukaguzi shuleni, tukafanya research through countrywide, tukazungumza na walimu wetu wanaofundisha madarasa haya ya form three na form four, watasema hawa zile topics ambazo zinawasumbua zile tukatengenezea module, tukaandaa in service training kwa walimu wetu ili kuwa upgrade waweze kufundisha grade ile ya form three na form four. Kwa kufanya hivyo ninaamini kwamba hizi “F” nyingi kabisa zingepungua. Huo ulikuwa mchango wangu wa mwanzo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wa pili, sayansi inakufa mashuleni, kwenye shule za sekondari hizi ukiangalia matokeo ya wanafunzi wa form four hata form six hawa wanaenda form six zaidi ya asilimia 70 wanasoma arts, hata wale wengine ambao form four walisoma sayansi. Kwa hiyo, kwa kipindi sasa hizi subject za sayansi zinaendelea kufa na zinakufa kifo kibaya. Sasa tutafute namna hapa ya kuweza kuwasaidia hawa vijana na hizi science subject. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye shule zetu hizi na ni-declare interest mimi mwenyewe ni mwalimu wa sayansi na nimefundisha zaidi ya miaka 25 katika shule hizi za Serikali, kwa hiyo, kuna matatizo tunayaelewa. Kuna uhaba mkubwa sana wa laboratory, achilia mbali hata vile vifaa vya kuviweka. Lile jengo angalau tukipata at least tube moja tuweke tunakosa hizi laboratory, sasa huwezi kufundisha sayansi without laboratory. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, saa nyingine mwalimu mwenyewe, kuna wakati mmoja alikuja mwalimu pale katika shule ananiuliza hii variable mass ndiyo ikoje, yeye ni mwalimu lakini kwa kuwa ni mwalimu mgeni na hakupata vizuri practical wakati akiwa anasoma kwa hivyo anashindwa hata baadhi ya terminology zinazotumika kule maabara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaishauri Serikali itafute namna ya kuweza kuziboresha hizi laboratory zetu ili tuihuishe sayansi. Huko tunapokwenda kwenye nchi ya viwanda, viwanda vinahitaji wasomi waliosoma sayansi baadae wapelekwe kwenye kusoma ufundi, baada ya kufaulu vizuri katika kiwango cha form four na form four six, kama hii sayansi itaendelea kulemazwa hivi sijui itakuwaje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kauli mbaya tunayopenda sana kuitumia Watanzania kwamba kilimo kwanza, mimi siyo muumini wa kauli hii, mimi nasema elimu ni mwanzo. Juzi moja nilikuwa nasoma gazeti wenzetu Afrika ya Kusini hivi karibuni tu kama hawajarusha watarusha satellite moja kubwa sana… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)