Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Kagera ni wakulima wa zao la ndizi, ni zao la chakula pamoja na biashara. Mkoa huu umeanza kulima zao hilo toka mwaka 1952 likitokea nchini Uganda, hii ni enzi ya ukoloni. Serikali ilitunga sheria ya kuwabana wananchi ili kutokomeza ugonjwa huo wa mnyauko ukawa umetoweka lakini ukajitokeza tena mwaka 2006 katika Wilaya ya Muleba na Kata ya Izigo sasa umeenea Mkoa mzima wa Kagera pamoja na Kigoma, Geita, Ukerewe na Kyerwa. Karagwe ni asilimia 70, Bukoba Vijijini ni asilimia 65, Misenyi ni asilimia 55, Ngara ni asilimia 35 na Biharamulo ni asilimia 25. Serikali ijue ugonjwa huo umeenea kwa asilimia 85. Je, ni lini Serikali itatuletea wataalam wa kuweza kutoa elimu juu ya ugonjwa huu ili wananchi waendeleze kilimo hiki hasa ikizingatiwa kuwa ni zao la biashara na chakula?
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Kagera kuna wafugaji wengi lakini hawana faida na ufugaji wao ukizingatia sasa hivi kuna ufugaji wa kisasa wa kunenepesha ng‟ombe. Je, ni lini Serikali itatuletea viwanda hasa kiwanda cha kuchakata maziwa, nyama na ngozi? Tunaomba Serikali itukumbuke Mkoa wa Kagera kuondoa umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, vijana wanajiajiri kuvua samaki na zana wanazotumia kuvua samaki wananyang‟anywa na kuchomwa kwamba ni haramu. Je, kama ni haramu zinatoka duka au kiwanda gani? Kwa nini Serikali isifungie kiwanda ambacho kina zana haramu? Badala ya kuwakamata wale wanaoingiza na kuuza wanakamata wanaovua si kuwaonea?
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia kwenye hotuba ya Waziri anasema anatoa elimu kwa wavuvi, je, Mkoa wa Kagera wamepata wangapi hiyo elimu? Tunaomba elimu hiyo itolewe ili vijana wafaidike na Ziwa lao Viktoria. Mkoa wa Kagera tuna kiwanda kimoja cha samaki, je, ni lini Serikali itatujengea kiwanda kingine ili vijana wapate ajira na wafaidikie na rasilimali ya nchi yao?