Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Susanne Peter Maselle

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SUSANNE P. MASELLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia katika hii Wizara ya Elimu. Nitaenda moja kwa moja kwenye hoja zangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu mikopo ya elimu ya juu. Kumekuwa na malalamiko mengi sana ya vijana wetu kutopata mikopo na hata kama wakipata mikopo hiyo kwa mwaka wa kwanza, mwaka unaofuata wanakosa sifa kutokana na kwamba masharti yamekuwa yakibadilika kila wakati. Kila mwaka Serikali imekuwa ikija na masharti mapya. Hali hii inamfanya kijana anashindwa kusoma na ku-concentrate katika masomo yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niishauri Serikali, naomba masharti haya kabla hawajayatoa wayalete hapa Bungeni ili tuweze kuyajadili maana yamekuwa yakibagua wanafunzi wetu. Mwanafunzi anakuwa na uhakika wa kusoma mwaka mmoja, mwaka wa pili anajikuta anakosa sifa kutokana na masharti ambayo yanabadilika kila wakati na yanamfanya anashindwa kuendelea, anabaki kutangatanga. Matokeo yake sisi Wabunge ndiyo tunakuwa kama msaada wa hao wanafunzi maana wanashindwa kuendelea na masomo kwa sababu sifa zimemwondoa moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu asilimia 20 ya bajeti ya Serikali. Iliamuliwa kwamba asilimia 20 ya bajeti ya Serikali iwe inaenda Wizara ya Elimu, lakini mpaka leo hakuna pesa ambayo inatolewa kwenye hiyo bajeti. Bajeti ya mwisho kabisa ambayo ilitoa hiyo asilimia 20 ilikuwa ni bajeti ya mwaka 2008/2009 kipindi cha JK. Sasa sasa hivi mnajigamba kwamba mnakusanya pesa nyingi, lakini hatuoni hizo pesa zikienda huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri akija hapa atuambie hizo pesa zitakwenda lini kwa sababu pesa hizi kwa mfano zingeenda kila mwaka zingesaidia sana changamoto hizi ambazo zinawapata walimu, kununua vitabu, kujenga maabara na kutengeneza mazingira mazuri ya wanafunzi. Lakini tumekuwa tukipiga tu mark time tunakwepa hili jukumu letu. Waziri anapokuja hapa naomba atuambie hiyo hela itaanza kwenda lini kwa sababu tunaenda kupitisha bajeti ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu madai ya walimu. Wengi wameongea hapa, mwaka jana tulipitisha bajeti lakini bado walimu hawajaanza kulipwa na wana malalamiko mengi sana. Sasa hivi tunaenda kupitisha bajeti, naomba Waziri akashughulikie madai haya kwa sababu walimu wetu wamekuwa wakihangaika sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri alishakuwa mwalimu anajua kabisa changamoto zinazowakuta walimu. Sidhani kama na yeye alipata matatizo haya. Inawezekana labda alipata matatizo haya ndiyo maana analipiza kisasi labda niseme hivyo kwa sababu ni kwa nini sasa tunapitisha bajeti na hashughulikii matatizo yao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie wanafunzi wetu. Wanafunzi wengi hawana madawati kwa maana kwamba shule nyingi hazina madawati. Tunaomba hiki kilio kiishe maana malalamiko yamekuwa mengi sana, naomba hiki kilio kiishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu capitation grants. Mheshimiwa Tunza amezungumzia, lakini mimi ningeenda moja kwa moja kwenye Mkoa wangu. Nataka hii shilingi 4,000 ambayo ilikuwa inabaki kwenye Halmashauri kwa ajili ya kununua vitabu waniambie wameifanyia nini kwa sababu vitabu vyenyewe hawajanunua, sasa wameipeleka wapi. Nataka wananchi wangu wa Mkoa wa Mwanza hasa shule zangu za Mkoa wa Mwanza waambiwe kwa nini hiyo pesa haikununua vitabu na imeenda wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi.