Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Ally Yusuf Suleiman

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mgogoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. SULEIMAN ALLY YUSSUF: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza napenda nimshukuru Mwenyezi Mungu Subhanahu-Wataala kwa kunipa afya njema na kuwepo hapa leo, na namswalia Mtume Mohamad Swalallahu Alayhi Wassallam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo, mimi nina mambo machache sana tu ya kuzungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, kila matokeo ya form four na form six yanapokuja kwa upande wa Zanzibar inakuwa ni vilio tu, hakuna vicheko kabisa kabisa. Tukiziangalia katika shule ambazo zinashika mkia zile shule 10 bora zinazoshika mkia basi kati ya sita mpaka saba zinatoka Zanzibar.

Mheshimia Mwenyekiti, tunataka kujiuliza Wazanzibar kwa nini kila siku tunafanywa kuwa watu wa daraja la pili? Ni kwa nini inakuwa hivyo? Na ikiwa masuala ya elimu ya juu ni masuala ya Muungano, naiuliza Wizara ni jitihada gani ambayo inachukua kuweza kuisaidia Zanzibar kuepukana na udhaifu ulio mkubwa kiasi hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia nijue hivi katika Bodi ya Mitihani, katika Bodi ya Wakurugenzi ile Bodi ya Mitihani kweli tuna wawakilishi kutoka Zanzibar pale? Mara nyingine inawezekana sababu ya udhaifu huu ni kwamba hakuna watu ambao wanaweza wakaishauri bodi vizuri katika masuala ya Zanzibar. Nataka Waziri aje anieleze kweli tunao watu pale? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ninataka nilijue kwa kifupi tu ni suala la mikopo. Bodi ya Mikopo imekuwa siku zote ikitoa mikopo kwa upande wa wanafunzi wa Zanzibar. Lakini mpaka hivi sasa hatujui haki ya Zanzibar katika mikopo ile ni kiasi gani. Wazanzibari ni asilimia ngapi tunapata? Kwa sababu tukijua hili itasaidia kuondoa yale malalamiko ambayo yako kwa wanavyuo wa Zanzibar kwamba Wazanzibari hatupendwi, Wazanzibari tunadhulumiwa. Hebu tuambieni Mheshimiwa Waziri, ni asilimia ngapi, tunataka kujua asilimia yetu katika Bodi ya Mikopo ni kiasi gani ili kuondosha haya malalamiko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia Mheshimiwa Waziri atakapokuja atufahamishe kati ya wanafunzi 122,623, Wazanzibari wangapi ambao wanapata mikopo miongoni mwao? Kati ya hao Wazanzibar ni wangapi? Kadhalika kuna wanafunzi 350 ambao wanasomeshwa nje kwa kupewa mikopo, nataka nijue kati ya hawa 351 Wazanzibar ni wangapi ili tujue haki yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala dogo pia nataka nilijue, ni kwa nini Wazanzibari hawapati grade A katika hii mikopo, wote ni B, C na kwenda chini. Ni kwa nini Wazanzibar hawapati nafasi hiyo ya kuwa full sponsored badala yake ni wa upande mmoja tu ndio ambao wanapata? Nataka uje unijibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakwenda haraka haraka tukija upande wa TCU. Upande wa TCU umeandika kwamba katika kazi zake ni kuhakiki ubora wa elimu na kuidhinisha programu zifundishwazo. Nataka kujua ni kwa nini TCU au TCU imeona nini katika elimu za dini? Elimu za dini hapa nijuavyo zinasomeshwa katika Chuo cha Muslimu University (MUM) na pia kinasomeshwa katika Chuo cha Abdulrahman Sumait kule Zanzibar. Lakini hawajaidhinisha chochote ni udhaifu gani waliouona au ni kitu gani kibaya… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji