Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa kunipatia nafasi. Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema kuweza kusimama hapa kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Elimu. Pia natoa pole kwa Watanzania wote waliopata mafuriko wakafiwa na wapendwa wao pamoja na kupoteza mali zao. Baada ya kuzungumza hayo sasa naanza kuchangia hotuba hii iliyopo mbele yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuulize ni jambo gani linalotupa kuteremka kiwango cha elimu katika nchi yetu? Tuna changamoto kubwa sana ndiyo inayoleta kuporomoka kwa elimu.

Changamoto ya kwanza ni upungufu wa walimu. Tuna upungufu mkubwa wa walimu, ukosefu wa vitabu vya kusomea na vitabu vya kujifunzia, maslahi ya walimu ni madogo na wanafundisha kwa muda mrefu bila ya kupandishwa daraja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba wapandishwe madaraja na waongezwe maslahi yao kwa sababu mama ikiwa hashibi hawezi kutoa maziwa ya kumlisha mtoto wake. Kwa hivyo ni lazima tuwaangalie kwa jicho kubwa ili waweze kufanya kazi zao vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuna ukosefu wa matundu ya vyoo pamoja maji. Hilo ni tatizo kwa sababu maji ndiyo uhai wa binadamu. Leo watoto wengi wa kike wanafeli kutokana na kwamba wakiwa katika siku zao za hedhi kuwa hawawezi kuhudhuria masomoni muda wa wiki moja mpaka wiki mbili. Hiyo inachangia watoto wa kike kufeli, kwa hivyo ni lazima Serikali liitatue kwa haraka tatizo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa walimu na hasa walimu wa sayansi. Tuna upungufu wa walimu wanaofika 15,968; huo ni upungufu kubwa sana. Tunataka nchi ya viwanda tutakwendaje kwenye viwanda ikiwa hatuna wasomi wa sayansi na ukiangalia upungufu mkubwa nao uko katika shule za msingi; kwa hiyo, ni lazima Serikali iajiri walimu mara moja kuziba mapengo ya wale wa vyeti fake waliotolewa na tupate walimu wa kuendeleza elimu ili elimu yetu iweze kupanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za Serikali zinasomesha lugha ya kiswahili wenzangu wengi wamezungumza. Lugha ya kiswahili kuanzia chekechea mpaka darasa la tatu. Wakati ni tofauti shule za private zinasomesha lugha ya kiingereza kuanzia chekechea mpaka darasa la tatu. Ukiangalia mtihani wao uko sawa sawa, je, watakuwa sawa hao kwenye matokeo wakati wale wameshaiva, wale ndiyo kwanza wanaanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo natoa ushauri kwamba Serikali ikae na wadau wa shule za private ili kushirikiana na kutoa elimu iliyo bora ili wote wafaidike kwa sababu wote ni watoto wa Tanzania na wote ni watoto wetu, tusibague wale wakawa bora kwetu sisi wakawa si bora. Leo inafika hadi shule za Serikali darasa la saba mtoto hajui kusoma wala kuandika, hili ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze kuhusu mitaala. Kila baada ya kipindi mitaala inabadilika. Inapobadilika tunawapa mzigo wazazi kwa sababu itabidi wanunue vitabu vipya. Wanaponunua vitabu vipya wengine wahana uwezo utawakutia watoto watano wanasomea kitabu kimoja, hilo ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tunawapa mzigo mkubwa walimu, kwa sababu mwalimu lazima kwanza ajifunze mtaala ule ndipo aweze kufundisha. Kwa hiyo, nashauri angalau miaka 10 ndipo baadae mtaala uangaliwe na kufanya tathimini kwamba je, mtaala huu utaendelea au mtaala huu bado haufai ili ubadilishwe ili kuwaondoshea mzigo walimu na wazee? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia kuhusu watoto wenye hali ngumu. Tukiangalia hapa Dodoma ukienda paleā€¦ (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)