Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kutoa mchango wangu katika hotuba hii ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuwa hapa leo, pia kwa kutulinda sisi sote Wabunge na kuwa hapa leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna ya pekee kabisa nimpongeze sana Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri sana anazofanya. Ninamuombea kwa Mwenyezi Mungu azidi kumuongoza, amlinde, amtunze na ampe maisha marefu. Nimpongeze Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Baraza lote la Mawaziri kwa kazi nzuri sana wanazozifanya. Nimpongeze sana Waziri wa Elimu, Mheshimiwa Ndalichako kwa hotuba nzuri. Pia nimpongeze Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Naibu Waziri na watendaji wote wa wizara kwa kazi nzuri sana wanazozifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo naomba nichangie sasa kuhusu elimu katika Mkoa wa Geita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kuweza kutenga fedha kwa ajili ya kukarabati shule kongwe hapa nchini. Kazi iliyofanyika na inayoendelea kufanyika katika kukarabati shule kongwe hapa nchini ni nzuri mno na inafaa kupongezwa na kila Mtanzania anayependa maendeleo. Hongera sana Serikali, hongera sana TAMISEMI na hongera sana Wizara ya Elimu kwa kuweza kusimamia vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee upungufu wa walimu katika Mkoa wangu wa Geita. Katika Mkoa wa Geita shule nyingi za msingi hazina walimu wa kutosha hivyo kupelekea walimu wachache sana na sera yetu ya elimu inasema mwalimu anatakiwa afundishe wanafunzi 45, lakini kwa mapungufu yaliyopo katika Mkoa wa Geita mwalimu mmoja anafundisha wanafunzi 100 mpaka 150. Kwa hiyo, kwa kweli ni changamoto, niombe sana Serikali iweze kutupatia walimu wa kutosha kulingana na mahitaji yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile katika shule zetu za sekondari za kata kuna mapungufu makubwa sana ya walimu na hasa walimu wa sayansi. Hatuwezi kufikia uchumi wa kati bila kuwa na walimu wa kutosha wa sayansi. Hivyo niombe sana Serikali iweze kuliona hilo watupatie walimu wa kutosha katika Mkoa wa Geita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna upungufu wa nyumba za walimu na mabweni, changamoto hii ni kubwa sana. Mwalimu anapokuwa mbali na kituo chake cha kazi hukupelekea kuchelewa kufika kazini, matokeo yake shule huwa chini ya kiwango. Niombe sana Serikali, mimi nishauri kwa nini tusitumie Shirika letu la Nyumba kuweza kujenga nyumba za walimu pamoja na mabweni ili kuondoa kabisa tatizo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo lingine la walimu kutopanda madaraja. Kuna walimu morale ya kufundisha inashuka kutokana na kutopanda madaraja kwa wakati. Mwalimu anapokaa kwenye daraja moja mwaka mmoja mpaka miaka mitano bila kubadilishwa kwa kweli inakatisha tamaa, matokeo yake walimu wanashindwa kufundisha vizuri. Mimi niombe Serikali iweze kuona inafanyaje ili walimu hawa waweze kupandishwa madaraja kwa wakati unaofaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja