Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MWITA C. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Polisi wamefanya kazi sana, ila wamefanya kazi vibaya sana. Kazi wamefanya, lakini wanafanya mbaya, ndiyo maana watu wanalalamika. Ni muda tu mfupi lakini kwa kweli Wizara hii mambo ambayo yamefanyika ni mengi sana na mengi yake ni mabaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ndugu yangu, asikilize tunachokizungumza hapa. Inawezekana watu wanaingiza siasa katika mambo ya msingi katika maisha ya watu, ni bahati mbaya sana. Tunatarajia Mheshimiwa Mwigulu Nchemba atakapokuja hapa kuhitimisha hoja, aje atueleze zile CCTV Camera ambazo zilikuwa kwenye nyumba ambayo ndugu yake Mheshimiwa Lissu wa Singida alikuwa anaishi, nani aliziondoa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia aeleze upelelezi umefika wapi? Muhimu sana. Hili jambo halihitaji siasa. Huyu mtu amelalamika kwamba anafuatiliwa na magari, akataja mpaka namba ya simu, akataja hata namba ya gari. Mheshimiwa Mwigulu Nchemba hajawahi kusimama hadharani na akawaeleza Watanzania, nani alikuwa na gari ile? Wale ni akina nani mpaka leo! Sidhani hata ndugu yake Mheshimiwa Lissu kama pole alimpa. Sina hakika kama ametoa hiyo pole kwake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, yako mambo yanazungumzwa hapa; tumezungumza juzi, Mheshimiwa Heche amezungumza akaomba Mwongozo hapa kwenye Bunge hili, kwamba Mbunge anasema ametishiwa maisha. Hawa watu wanapiga simu, wakati mwingine wanaandika message.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa Polisi ukiandika maneno yenye ukakasi kwenye mitandao, unafuatiliwa popote ulipo, unawekwa ndani, kizuizini. Hawa ambao wanatuma message za kwamba “nitakushughulikia;” “nitakuonyesha;” “utanikoma;” kwa nini hawashughulikiwi? Mheshimiwa Heche alilalamika hapa Bungeni, lakini bahati mbaya naona haya mambo yamebadilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mwigulu Nchemba aseme, yule ndugu yake John Heche, Ndgu Chacha Suguta ambaye amezikwa leo, yule bwana amekamatwa na Polisi akapigwa pingu. Hapo ndipo watu wanahoji maadili ya Polisi. Hata kama sio wote, watu wanahoji inakuwaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi aliyefundishwa, ameenda Chuo cha Mafunzo kule Moshi au elsewhere, anamkamata mtuhumiwa aidha ana makosa au hana makosa; wala hata hakuua; au hata kama ni muuaji, Mahakama ndiyo ina wajibu wa kusema huyu ahukumiwe kiasi fulani au apewe adhabu gani. Anapigwaje kisu? Hiyo kauli ni lazima ichukuliwe kwa uzito wake katika Taifa hili na iwe fundisho na matukio mengine ambayo yanafafana na hayo. Hayo ni mambo ambayo kwa kweli yanahitaji kuangaliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba alizungumza kwamba kuna watu wanaokotwa kama jambo la kawaida. Hii hali ya watu kuamka asubuhi amekatwa mapanga kama yule wa Kilombero, kama dude la mgomba, halafu watu wanaona, watu wanaokotwa kwenye mifuko ya sulphate kwenye kingo za bahari kama mambo ya kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo haya mnazoeza Watanzania mauaji, itafika mahali kuanza kuona siyo jambo la ajabu ajabu sana. Mwingine anasimama hapa mtu mzima kabisa anatwambia kwamba eti kwa sababu idadi ya Wapinzani ni chache kuliko ya CCM; so what? Yaani unahalalisha uhalifu kwa idadi ya watu, kitu ambacho hakikubaliki. Yaani mtu sikutarajia anaweza kuongea kitu cha namna hiyo ambacho kimsingi ni jambo ambayo haliruhusiwi kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachosema, Polisi wamefundishwa. Polisi wanalipwa kodi ya Watanzania; Polisi viatu wanavyovaa ni kodi yetu, chakula chao ni nguvu yetu; nguo wanazovaa ni sisi; wafanye kazi kwa uadilifu, wafuate maadili yao. Hiyo ndiyo hoja ya msingi hapa. Hatusemi wamfuatilie mtu yeyote yule. Kamata mtu yeyote ambaye ana makosa yaliyothibitishwa apelekwe Mahakamani ahukumiwe. Siyo ku-retain watu katika retention kama ilivyo kwa wale Mashehe. Ni makosa makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, hivi sisi tunachangisha kujenga Vituo vya Polisi; pale Chanika tumejenga. Hawa Polisi tunajenga pamoja nyumba na Vituo vya Polisi, hawana magari. Kwa nini magari ya washa washa yale msiyabadilishe yawe magari ya kufanya patrol kwenye vituo vyetu ambako kuna kuna raia? Ujambazi unafanyika, hawana mafuta ya kufanya patrol, lakini magari ya washa washa yapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, ndugu yangu na mjukuu wangu, nilishangaa sana. Jeshi la Polisi nchi hii, ndugu y angu Sirro, kaka yangu wa kule Musoma, anafanya maandamano ya magari kwenye mikoa nchi nzima kwa Mange Kimambi? (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani they are not serious, yaani mtu yuko Marekani, anaandika maneno kwenye mtandao, tutaandamana tarehe 26. Wamekamata vijana wetu nchi nzima, wanawapiga. Mange Kimbambi, kweli! Haki ya Mungu mimi nisingehangaika naye. Nilikuwa nawashangaa hapa Wabunge wa CCM kuwe na maandamano kwa hoja ipi? Nani anaandamana? Sisi tulikuwa hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukitaka kuandamana tutakaa vikao, tutaitishana, hakuna Mbunge wa Upinzani atabaki humu ndani. Tutakwambia weka barabarani majeshi, weka maji ya kuwasha, weka bunduki, piga risasi, ua unayeua, atakayebaki ataandamana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nadhani mnahitaji kutumia akili sana.