Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja vya michezo mashuleni, viwanja vingi vya michezo nchini hasa viwanja vya shule vimechukuliwa na taasisi mbalimbali wakiwemo wanachama wa CCM, matokeo yake shule zinahangaika hakuna sehemu ya kuchezea watoto wa shule. Naomba Serikali ihakikishe viwanja hivyo vinarudishwa kwenye shule ili wanafunzi wetu waweze kuvifurahia. Kwa mfano, uwanja wa sabasaba ulioko Njombe uliochukuliwa na CCM, uko kwenye eneo la shule ya msingi ya Sabasaba na Mpechi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo mashuleni watoto wetu wa shule za msingi na sekondari wamelemaa, awali kulikuwa na michezo hata mchakamchaka lakini hivyo vyote vimefutwa, naomba Serikali irudishe mchakamchaka mashuleni na itiliwe mkazo somo la michezo na mazoezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maadili katika nchi yetu yameporomoka, naomba somo la maadili lifundishwe mashuleni kuanzia shule za msingi hadi vyuoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iwasaidie wasanii kuboresha kazi yao badala ya kuwaadhibu kwa kuwafungia. Tutoe maelekezo vizuri badala ya kutumia nguvu, pia tusiache wasanii kuonesha sanaa zao kama nyimbo kwa muda mrefu halafu baadaye tunawafungia wakati tayari watu wamekwisha sikia nyimbo hizo, tuwasaidie wasanii wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.