Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. GEORGE M. LUBELEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri yenye ufafanuzi. Pili, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Pamoja na kuunga mkono naomba nichangie maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja vya mpira (football) kwa kuwa viwanja vinamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) hivyo vina hali mbaya sana vinatakiwa ukarabati na CCM haina fedha za ukarabati. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa ruzuku kwa Chama cha Mapinduzi ili kuvikarabati viwanja vyake hasa ukuta eneo la Pitch ili timu zetu za ligi kuu ziweze kuchezea viwanja hivyo bila shida yoyote?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waandishi wa Habari wa Umma (Serikali) kwa kuwa sekta ya habari ni muhimu sana kwa maendeleo na uchumi wa nchi yetu, Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Waandishi wa Habari kila Wilaya ambako wapo wananchi wengi na wanafanya kazi za kilimo na shughuli nyingi za maendeleo kwa ajili ya kuinua uchumi wa wananchi. Vyombo vingi vya habari vinahamasisha sana wananchi kushiriki shughuli nyingi za maendeleo badala ya Waandishi wa Habari kujazana Mijini tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyombo vya Habari hasa vya Serikali havipati maslahi ya kutosha kama vile TBC maslahi ni kidogo sana ndiyo maana watumishi wengi wanahamia vyombo binafsi ambao wanalipwa vizuri. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha maslahi ya watumishi wa TBC na Waandishi wa Habari wa Serikali ambao wapo chini ya Idara ya Habari?

Mheshimiwa Mwenyekiti, timu nyingi za mpira wa miguu zina migogoro mingi sana. Je, ni sababu zipi zinazosababisha migogoro hiyo na kusababisha kushuka kiwango cha mchezo wa mpira wa miguu hapa Tanzania? Je, Serikali itasaidiaje kupunguza migogoro hiyo ili kuboresha soka la Tanzania hata Kimataifa.

Mheshimiwa naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.