Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa mchango wangu kidogo katika Wizara hii muhimu katika kuendeleza michezo na utamaduni katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, Sera ya Sheria ya Utamaduni inayotumika nchini kwa sasa imepitwa na wakati ndiyo maana tunashuhudia migongano na mivutano hasa katika tasnia zingine sanaa zikifungiwa kwa maelezo ya kufanyika kinyume na maadili tuliyokubaliana ambavyo vinatumika kuamua huyu kakiuka maadili na huyu hajakiuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tumeona hata baada ya baadhi ya kazi za sanaa kufungiwa kumekuwa na malalamiko kuwa mbona baadhi ya kazi za sanaa ambazo zinaonekana kuwa na migogoro kuliko zilizofungiwa bado zipo na zinatumika. Hii inaonesha upo umuhimu wa kupitia upya sheria na sera za utamaduni nchini ili kulinda na kutunza utamaduni wetu na kazi zetu za sanaa bila uonevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili, ipo haja ya kupitia upya sheria na taratibu zinazotumia mwenendo wa vyombo vya habari vya ki-electronic yaani TV na Radio katika mazingira ya teknolojia ya leo unapofungia TV na Radio za nchini kwetu kwa sababu ya kupiga muziki fulani (kutumia kazi fulani za sanaa) wakati huo huo ving’amuzi vyetu nchini vinaonesha channels za nje ya nchi ambazo hatuna uwezo wa kuzuia uoneshwaji wake nchini ni sawa na kuvinyima vituo vyetu vya TV hapa nchini vishindwe kushindana kwenye ushindani wa soko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, kama kweli tunataka nchi yetu tusomeke kwenye dunia kwenye michezo ni lazima Serikali ikubali kuwekeza katika michezo, tusipofanya hivyo tutaendelea kuwa wasindikizaji katika michezo tutakayokuwa tunashiriki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali lazima tukubali kushirikiana na Wafadhili wanaofadhili timu zetu kuhakikisha timu zetu zinapata muda mrefu wa kukaa kambini ili waweze kufanya mazoezi ya pamoja. Tusipofanya hivyo tutaendelea kuwa wasindikizaji kwenye kila mashindano. Pia tuwatie moyo wachezaji na wasanii wetu tusiwakatishe tamaa maana wengi wamefika hapo kwa juhudi zao wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.