Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Harrison G. Mwakyembe, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kazi nzuri iliyotukuka. Naipongeza Wizara kwa kazi nzuri, hotuba na Mipango mizuri, hivyo naunga mkono hoja hii kwa furaha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, chemchemi ya michezo ni vijana wetu vijijini. Chemchemi hii ikihifadhiwa, ikaendelezwa huliletea Taifa sifa na faraja ya kushinda katika mashindano ya Wilaya, Mkoa, Taifa na Kimataifa. Kwa sababu hiyo niliomba na bahati nzuri nikaahidiwa na Waziri tangu Mei, 2016 mipira 100 football kwa ajili ya kuendeleza mpira wa miguu ngazi ya Kata. Mipira hii niliahidiwa na Waziri wakati huo 2016 kama mchango wa kuendeleza League ya mpira wa miguu Wilayani Mwanga (Maghembe Cup).

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri anikumbuke kutekeleza ahadi yako hii.