Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. DEO F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Matangazo ya shirika hili la utangazaji la Taifa hayafiki katika Wilaya ya Ludewa na maeneo mbalimbali ya Ludewa. Hivyo tunaiomba Wizara kuangalia suala hili ili Ludewa ipate matangazo ya TBC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umefika wakati sasa wa kuwa na utaratibu wa mpango wa kujua matangazo ya TBC juu ya uwekaji wake awamu kwa awamu katika maeneo mbalimbali ya nchi. Hii itaondoa usumbufu wa kuulizauliza lini itakuwa ni zamu ya maeneo fulani na pia kujua TBC itachukua muda gani kufika nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vazi la Taifa. Kuna mchakato ulianza wa Vazi la Taifa, lakini mpaka sasa hakuna mwendelezo wowote wa kupatikana kwa vazi hilo. Vazi hilo ni muhimu kwani linaweka utambulisho wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maandalizi ya Timu Zetu katika Mashindano ya Kimataifa. Serikali itenge pesa za kutosha katika maandalizi ya michezo mbalimbali katika fani za mpira wa miguu, pete, wavu na kadhalika kabla ya kwenda katika mashindano mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ajira za Maafisa Michezo na Utamaduni. Serikali haitengi bajeti kwa ajili ya ajira za Maafisa Utamaduni na Michezo katika kuibua aina mbalimbali za michezo. Ukitoa soka na riadha bado tuna michezo mingi sana, ipewe kipaumbele. Kwa mfano volleyball, tennis, basketball, tufe na kadhalika.