Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Wizara. Hongera sana kwa timu nzima kwa kazi nzuri, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu, wataalam na wasaidizi wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maeneo ya Kihistoria, Utamaduni, Mila na Desturi. Eneo la Masonya Wilayani Tunduru ni tajiri sana kwa mahitaji haya. Ni ombi langu eneo hili liboreshewe miundombinu yake, kutangazwa na kuendelezwa kushirikiana na Wizara yenye dhamana ya malikale na utalii ni muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema kushirikisha machifu katika Wilaya ya Tunduru. Chiefdoms bado zina wazee wenye taarifa kubwa na muhimu, licha ya taarifa kutoka halmashauri ya wilaya; Chief Mataka, Chief Ntalika, Chief Kanduru, Chief Mbalamula, Chief Nakoko, kwa kuanzia. Ni vizuri hatimaye huko siku zijazo tukawa na orodha, directory ya maeneo haya muhimu yote na ikazinduliwa kwa matumizi ya kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika, Ukombozi wa Kusini mwa Afrika hauwezi kuzungumziwa ukakamilika bila kutaja Wilaya ya Tunduru. Kituo cha Masonya ni maarufu kama kambi ya kimkakati kwa harakati za ukombozi wa Msumbiji. Yapo makazi na maficho ya Samora Machel, Mwalimu Nyerere na wengineo. Nashauri Mheshimiwa Waziri atembelee kambi hii tukiongozana nami, ili aone umuhimu wa eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Usikivu wa Redio (TBC). Kukatikakatika na kupotea kwa matangazo, pia usikivu hafifu katika baadhi ya nyakati ni mambo yanayowakera wananchi wa Tunduru. Tunaomba ufuatiliaji na ufumbuzi wa tatizo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maadili, utamaduni, mila, desturi katika Wilaya ya Tunduru huenda hili likawa ni tatizo la Taifa zima. Vinaathiriwa na maendeleo ya sayansi na teknolojia, hususan, simu za viganjani, TV na kadhalika, kiasi ambacho hata vijijini ngoma za asili zinapotea maadili ya Mtanzania na makabila unapotea. Nini mkakati wa Serikali?