Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika masuala yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sekta ya Michezo, imekuwa ikikumbwa na changamoto ya gharama kubwa ya vifaa vya michezo inayotokana na kodi inayotozwa hasa vifaa vinavyotolewa kama msaada kwa mfano kulikuwa na nyasi bandia ambazo hadi sasa sijui suala hilo limefikia wapi kwani zilizuiliwa bandarini. Waziri atupe majibu ya suala hilo. Kuna uvamizi na kubadilishwa kwa matumizi ya viwanja vya michezo. Serikali itupe majibu na pia kuna uvamizi wa maeneo yaliyotengwa kwa burudani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo ni biashara, hivyo ni lazima tufanye uwekezaji kama biashara yoyote inavyotakiwa ifanyike. Uwekezaji lazima uanzie katika ngazi ya chini kwa kutayarisha watoto wetu kuwa wachezaji wazuri kwa michezo mbalimbali au sanaa na utamaduni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shughuli za michezo na utamaduni katika halmashauri zinakuwa chini ya Idara ya Elimu msingi ambayo ina majukumu mengi ya kushughulikia elimu na sehemu kubwa ya bajeti yake matumizi ya kawaida inatoka Serikali Kuu. Kitengo cha michezo kinamezwa na shughuli za elimu, hivyo kushindwa kutimiza wajibu na majukumu yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri zile asilimia 10 za wanawake na vijana ziwekezwe kwa kuwapa mafunzo vijana na wanawake katika vyuo mfano, TASUBA ili wapate ujuzi na wawekeze katika sanaa. Halmashauri zinaweza kusomesha hata vijana wawili kila mwaka. Hii ni sawa na
kuwapa ndoano badala ya kuwapa samaki. Tusiwape fedha tu, mafunzo ni muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la Kilimanjaro Marathon. Michezo hii ilianza kufanyika Mkoa wa Kilimanjaro lakini pia Mkoa wa Mwanza wameanzisha marathon. Mapendekezo au ushauri wangu ni kuwa; Serikali iangalie namna watakavyogawa mikoa na shughuli mbalimbali na tofauti ili iweze kuwa tulivu. Mfano, Mikoa ya Kusini wanaweza kuwa na mashindano ya vifaa vya majini kama vile mashua na boti na mikoa mingine itafutiwe michezo kulingana na mazingira yake kama vile mashindano ya magari na kadhalika hii itasaidia wananchi kujua na kutilia maanani sehemu ambayo mchezo anaoutamani na mahali atakapokwenda kufanyia ushindani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.