Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ZAINABU M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri Mheshimiwa Dkt. Harrison Mwakyembe pamoja na Naibu wake kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni yangu nashauri Serikali iwekeze katika mchezo wa mpira wa miguu pia isisahau kuwekeza katika michezo mingine ambayo tayari imeshiriki katika mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi yetu na imesajiliwa, kufuata taratibu zote za kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Roll Ball – Timu hii ya mchezo wa Roll Ball imeshindwa kushiriki kwenda kuwakilisha nchi katika nchi ya Kenya kwa sababu ya kukosa wadhamini. Hivyo Serikali ione haja ya kusaidia mchezo huu ambao utasaidia kuleta ajira pia kusaidia nchi kujitangaza Kimataifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu itolewe kwa wasanii wetu hususan wanaoimba muziki wa kizazi kipya, kuweza kutunga na kuimba nyimbo zenye maadili yanayoendana na utamaduni wa nchi yetu. Serikali itunge sheria ya kudhibiti vijana ambao wanavaa nguo fupi (nusu uchi) ambazo haziendani na maadili yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali, iweke mkakati maalum wa kuhamasisha michezo mashuleni, kuanzia shule za awali, shule za msingi, sekondari hadi katika vyuo ili kuweza kuibua vipaji kwa vijana wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uwanja wa Taifa upo katika Wilaya ya Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam, hivyo pindi mechi zinapochezwa katika uwanja huo wananchi wa Wilaya ya Temeke hawafaidiki na fedha zinazopatikana katika viingilio. Hivyo naishauri Serikali kwa kushirikiana na TFF iweze kutoa kiasi cha fedha kwa Wilaya ya Temeke ambayo itasaidia katika kuboresha miundombinu na shughuli nyingine za kijamii katika Wilaya hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mungu awape afya njema Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake ili kuweza kutekeleza majukumu yao ya kila siku.