Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ili nami nichangie Wizara hii.

Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na Watendaji wote wa Wizara hii kwa kufanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ni Vyombo vya Habari. Vyombo vya Habari ni muhimu sana katika maendeleo ya nchi hii na uchumi wa nchi hii. Serikali ilikuwa hasa vyombo vya Habari vya Umma tulishalalamika hapa Bungeni kwamba habari nyingi zinazoandikwa ni za mjini tu, lakini vijijini ndiyo kuna taarifa nyingi, tulishauri Serikali kwamba, kila Wilaya iwe na Mwandishi wa Habari. Kwa hiyo, huo ni ushauri wangu Mheshimiwa Waziri, kule habari nyingi hazifiki kwenye vyombo vya habari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, maslahi ya vyombo vya habari. Vyombo vya habari vya umma kama alivyozungumza Mheshimiwa Mbunge mmoja vyombo hivi vinafanya kazi nzuri sana na vinailetea sifa nchi yetu, wanaandika taarifa kila siku tunasoma magazeti, habari tusingezipata bila yale magazeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyombo vya habari kwa mfano TBC, TBC ni chombo cha umma, lakini TBC inafanya kazi katika mazingira magumu sana. Kwanza vyombo vyao vimechakaa, baadhi ya vyombo kwa hiyo, kuna baadhi ya maeneo katika nchi hii TBC haisikiki. Kwa hiyo, Serikali ijitahidi kuongeza bajeti ili tuboreshe TBC iweze kusikika nchi nzima hasa TBC One pamoja na TBC Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maslahi. TBC wanafanya kazi usiku na mchana. Hapa tunaona wanavyohangaika usiku na mchana wanafanya kazi, lakini maslahi yao ni kidogo sana. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri aboreshe maslahi ya watumishi wa TBC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, viwanja vya michezo. Pitch ikiwa nzuri na timu itacheza vizuri mpira...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)