Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami niungane na wenzangu kumpa pole sana Mbunge mwenzetu John Heche kwa kufiwa na mdogo wake kwa kuchomwa kisu na Polisi kule Tarime.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze moja kwa moja kuchangia Wizara hii muhimu ambayo inahusisha Habari, Michezo, Utamaduni na Sanaa. Jambo la kwanza ambalo ningependa kuchangia leo ni kuhusu suala la Bunge Live. Bunge ni chombo muhimu sana cha uwakilishi, chombo kikuu cha uwakilishi wa wananchi hapa Tanzania na tunaamini Bunge ni kama mkutano wa wananchi wote kwa sababu kuna wawakilishi kutoka pande zote za Tanzania humu ndani ya Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo nadhani ilikuwa ni muhimu sana Serikali yetu iliangalie upya hili suala la kuondoa Bunge Live ili wananchi waweze kutuona wawakilishi wao tunavyowawakilisha ndani ya Bunge ili iweze kuwafikia moja kwa moja na kujua vitu gani vinavyoendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii nchi inaongozwa na Mihimili mikuu mitatu, kuna Serikali Kuu, Mahakama na Bunge. Tumeona jinsi ambavyo viongozi wa Serikali wakifanya ziara mara kwa mara na wanaoneshwa live maeneo mengine. Hii inaonesha ni jinsi gani ambavyo ni muhimu sana kwa

wananchi kuweza kuona viongozi wao wanafanya na kutekeleza vitu gani ambavyo wametutuma.

T A A R I F A . . .

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, sina haja ya kuijibu hiyo taarifa kwa sababu mimi naongelea Bunge Live yaani hapa ninavyoongea watu wawe wanashuhudia live kule, Dada yangu vipi? Hiyo saa tatu watu wanakuwa wamechoka, watu wanaangalia Bunge hadi usiku mkubwa na siyo live, hiyo ni recorded. Kwa hiyo, hilo lilikuwa jambo langu la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, wiki iliyopita niliongea jambo la msingi sana kuhusu Chama cha Mapinduzi kupora viwanja vingi vya michezo ambavyo vimekuwa vikimilikiwa na Serikali lakini sasa vinamilikiwa na Chama cha Mapinduzi na wameshindwa kuviendeleza. Hapa ninavyoongea na wewe ni kwamba hapo kwenye Kata ya Ruaha kwenye Jimbo la Mikumi kuna utata mkubwa na taharuki kubwa sana kati ya wananchi na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ambao kwa kutumia mabavu wameupora uwanja wa shule ya msingi Ruaha ‘A’ ambao pia unatumia na Ruaha ‘B’ pia unatumika na shule ya sekondari ya Kidodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sera ya elimu inasema kwamba kila shule lazima iwe na uwanja wa michezo. Pale Ruaha wanafunzi wa shule ya msingi Ruaha ‘A’ na Ruaha ‘B’ pamoja na shule ya sekondari ya Kidodi wanatumia uwanja huo, Chama cha Mapinduzi kimeupora na kinaanza kusema sasa hivi ni wa kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja huo ulijengwa mwaka 1986 ambapo wananchi walijitokeza na kufanya harambee kwa ajili ya huo uwanja na wakajenga vibanda pembeni ambapo mkataba walioingia na mkataba wanao mpaka leo inasema kwamba Serikali itamiliki ule uwanja lakini yale maduka ya pembeni yatakuwa ni haki ya wamiliki au wananchi ambao walikuwepo na mkataba wamesaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu cha ajabu juzi Chama cha Mapinduzi wamekuja pale Ruaha wakiorodhesha majina na kuwaambia wale wananchi waondoke. Kwa kweli kuna hali mbaya sana na niwambie kitu kimoja, iwapo Chama cha Mapinduzi kitafanikiwa kuchukua ule uwanja maana yake tunakwenda kufunga shule ya msingi Ruaha ‘A’, Ruaha ‘B’ pamoja na shule ya sekondari ya Kidodi kwa sababu hawana uwanja wa michezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka niongee kuhusu suala la BASATA, inasikitisha sana hii Wizara kwamba hadi sasa imetimiza asilimia 59 tu ya bajeti yake na asilimia 41 mpaka leo tunavyoongea haijakamilika. BASATA ni chombo cha msingi na tunaichukulia BASATA kama wazazi lakini BASATA imegeuka na kuwa kama chombo cha hukumu kwa Wasanii wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, BASATA ni kama mlevi na mtoto akijisaidia kwenye mkono wako huukati, unauosha na unaendelea na shughuli zingine. Niliamini kwamba BASATA inatakiwa iwape elimu hawa wasanii wa Tanzania waweze kujifunza, waweze kupata ushauri lakini pia waweze kuangalia jinsi gani ambavyo wanaweza kuisaidia tasnia ya muziki hapa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie wenzetu wamefanyaje, Uingereza kwa mwaka 2015 muziki peke yake umechangia GDP paundi bilioni 4.1 katika Pato la Taifa la Uingereza. Marekani mwaka 2015 muziki peke yake umechangia GDP ya dola milioni 15. Kwa hiyo, naamini kabisa kama Wizara inataka kuwekeza kwa vijana maana huwezi ukamkamua ng’ombe ambaye hujamlisha majani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwaambia Serikali waweke bajeti kwa wasanii, wana matatizo makubwa tofauti na hayo wanayoyafanya maana wanadhani kwamba kuwasaidia wasanii wa Tanzania ni kuwaalika sehemu za maofisi zenu kupiga nao picha, kupiga selfie na vitu vingine. Wasanii wa Tanzania wana matatizo makubwa, hawahitaji kula ubwawa na wao. Wanahitaji wawasaidie masuala ya kazi zao zinazoibiwa, wanahitaji wasaidiwe masuala ya masoko na mitaji. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaambie ndugu zangu, BASATA mpaka sasa katika hali ya kustaajabisha ndiyo imepewa mamlaka ya kusimamia hii kitu lakini bajeti yake ni milioni 23 kwa mwaka mmoja, mwaka 2016…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)