Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nami nafasi hii ya kuchangia asubuhi kwenye Wizara hii. Kwa sababu nina dakika tano, nitajitahidi niende haraka sana ili mambo yangu haya mtatu niweze kuyawasilisha vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, naipongeza hii Wizara kwa hatua ya kupitia ile sera ya mwaka 1995 na kuja ile ya mwaka 2017 ili iboreshe Sekta ya Michezo. Namwomba Mheshimiwa Waziri aikimbize sana, kwa sababu kwa hali jinsi iliyo tukakaa kama tulivyo kwa muda mrefu, Sekta ya Michezo itazidi kushuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ambalo ningependa niliseme asubuhi ya leo ni kuhusu kuwawezesha wale ambao wana nia ya kujenga viwanja vya michezo au sports facilities mikoani ili waweze kuifanya kazi hii vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kuna taasisi nyingi zina nia ya kujenga viwanja hasa kwa kutumia nyasi bandia, lakini changamoto kubwa wanayokutana nayo ni gharama ya kuweza kulipia ushuru ili zile facilities zije.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Wizara, ukienda pale Kidongo Chekundu, ukiangalie zile facilities zilizojengwa, tukipata vilabu vyenye uwezo wa kufanya hivyo, vikatengeneza, vikapewa msamaha wa zile nyasi bandia, nina uhakika viwanja vitakuwa bora zaidi na michezo itakua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo nataka niliseme, nchi yetu sisi hatuna Sports Academy, lakini ni wajibu wa Serikali sasa kuona namna gani tunatoka. Mimi nina ushauri, umefika wakati sasa Serikali ichague shule moja ya sekondari ya mkoa iipatie facilities na iwe na curriculum ya michezo tu, iwe na masomo saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika masomo hayo saba, ziwe lugha zote ikiwepo Kiswahili, Kifaransa, Kiingereza na Kispaniola halafu na somo la Historia, Geografia na Uraia. Yanatosha kabisa. Halafu vyama vya soka vikishirikiana na Maafisa Utamaduni watafute wachezaji kupitia UMITASHUMTA na UMISETA, hao waingie kwenye ile shule maalum ya michezo ya Mkoa. Tukifanya hivi, nina imani baada ya muda siyo mrefu, mambo yatakwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, naomba niliseme kwa kifupi tu. Hii wiki kuna sintofahamu iliyokuwa ikiongelewa humu Bungeni kuhusu umiliki wa viwanja vya michezo vinavyomilikiwa na Chama cha Mapinduzi. Naomba nitumie fursa hii kuliambia Bunge lako Tukufu, sera ya TANU mwaka 1957 ilikuwa ni kuboresha michezo. Pamoja na hilo, katika harakati zetu za kupata uhuru, Chama cha TANU kiliishirikisha Yanga na Simba katika vuguvugu la kuleta uhuru mpaka uhuru ukapatikana mwaka 1961. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia mwaka ule mpaka leo Chama cha Mapinduzi kimekuwa na sera kila kwenye tawi lao au kwenye Ofisi ya Mkoa kutenga eneo kwa ajili ya michezo. Hiyo kazi hawakuwahi kuicha. Kwa kukuthibitishia hilo, mlezi wa Yanga kwa kipindi kile alikuwa ni Mzee Karume na mlezi wa Simba alikuwa Mzee Kawawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1961 Tanzania ilikuwa katika mfumo wa vyama vingi, wala hakikuwa chama kimoja. Katika kipindi cha mfumo wa vyama vingi 1961 mpaka 1965 bado TANU iliendelee kuhimiza ukuaji wa michezo na maazimio ya kujenga viwanja vya mpira halikuwahi kuwa azimio la Serikali, bali lilikuwa ni azimio la Halmashauri Kuu ya TANU na baadaye Halmashauri Kuu ya CCM. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kuwaambia, mwaka 1992 tulipokwenda kwenye mfumo wa kurudisha vyama vingi kwa mara ya pili, waliotaka kwenda kwenye vyama vingine walikwenda kwa hiari yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilipata swali la kujiuliza, hebu tuulizane hapa Mheshimiwa Lwakatare alianza na CUF. Je, alipojenga zile Ofisi za CUF baada ya kuhamia CHADEMA anadai matofali ya Ofisi zake? Ni kitu ambacho hakiingii akilini. Ninachotaka kusema, sera ya michezo ni sera ya CCM.

T A A R I F A . . .

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, tatizo ni tafsiri tu. Kujenga au kununua ni wazi ilitokana na michango ya Wanachama. Hela za wanachama ndizo zilizojenga. Mchango wa mwanachama mmoja mmoja ndiyo uliojenga hizi facilities. Hii siyo hoja ya msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya msingi ni kwamba from day one, TANU ikiazishwa na CCM ilikuwa na sera mahususi ya michezo, ndiyo maana mpaka leo kila kwenye Ofisi ya CCM kuna kiwanja cha michezo. Hebu tuwaulize nyie wenzetu, kwenye Ofisi zenu mna hata yadi mbili za watoto kucheza kitenesi? Sasa kwa nini leo mnataka kudai viwanja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuwaambieni kitu kimoja, kukuthibitishieni kwamba michezo ni sehemu ya Chama cha Mapinduzi mpaka mwaka 1998 kwenye Katiba ya Yanga na Simba, viongozi wao, Marais wao walikuwa wanateuliwa na Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana wa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)