Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nilikuwa najaribu kuangalia kumbukumbu yangu kichwani, Serikali imewekeza pesa nyingi sana kwenye michezo hasa mchezo wa mpira. Nikirudisha memory zangu naona kama mpira wa miguu na michezo hiyo mingine haitusaidii sisi kama Serikali kutangazwa kwenye nchi nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijabu kuangalia, sisi inawezekana tuna bahati sana ya kutangazwa na wasanii hasa wa muziki na filamu. Wamefanya vizuri, tumeona leo hata ukienda huko nje kwenye clubs za Wazungu inapigwa miziki ya Kiswahili unapata morali hata wewe wa kuingia club na kucheza. Ila kwa style zinazoendelea kwa Mheshimiwa Waziri na yenyewe hii tasnia tunaenda kuipoteza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshuhudia sana hapa kipindi cha katikati fungia fungia. Msanii anafanya kazi yake nzuri; na wewe ni mpenzi wa muziki, nakufahamu. Kinachomfanya mtu ahamasike kulipa kiingilio kwenda kwenye muziki ni pamoja na matangazo mazuri atayokuwa ametangaza msanii. Kwa sasa kinachoendelea, msanii anafanya kazi nzuri, kwenye kushuti akikosea tu kidogo mpasuo, Mheshimiwa Waziri huyo, amefunga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka kumwuliza, anafungia miziki ya Tanzania au anawafungia wasanii wa Tanzania kupasua sketi kuonesha mpasuo, hebu aangalie miziki ya akina Rihana na ndiyo wanakaa wanaangalia humu kwenye youtube kila saa. Hii ya Tanzania ambayo mnataka wasanii wetu wavae sijui dela, sijui wavae pekozi, hakuna mtu aliye na hobby na miziki ya pekozi kwa sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia msanii anafanya kazi nzuri, ana-invest hela kwa mkopo na nini, akikosea tu mpasuo anafunga. Tukienda Samora, mbona akinamama tunaona kama zile nguo wanazovaa kule Samora Samora zinafafana tu na Wanamuziki, kwa nini kule hawapeleki kifungo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namshauri Waziri Mheshimiwa Mwakyembe, hebu tujifunze wasanii wetu wanaiga miziki ya Ulaya, halafu wanaiga na style za Ulaya na miziki Ulaya huwezi ukapeleka muziki mtu amevaa kanzu au dela haiwezekani!

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie faida tunazozipata kwa hawa wasanii wetu. Ni bora wakatafuta muda wakawapa semina kuliko kuwaacha, mtu anafanya kazi nzuri, anagharamika, halafu anakosea kosa moja tu, unamfungia miezi sita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niulize swali lingine, mwanamuziki ameimba muziki mwaka mzima na nusu, halafu Mheshimiwa Waziri anaibuka anasema huu muziki umekiuka maadili, anafungia. Sasa huko vijijini watu wameshaweka kwenye simu, kwenye computer, unapambana nao vipi? Anatupa shida sana sisi wenzake wa vijijini kwa sababu wana- create ujinga kwa watu walioko vijijini huko, Watendaji, akina nani, akikosa kazi tu anaanza kukamata computer zina miziki imefungiwa na Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri pia yeye ni mtu wa zamani kidogo ninavyomwona umri wake, hebu nataka anisaidie, vazi halisi la utamaduni wetu sisi la Kitanzania ni lipi? Kwa sababu nakumbuka wale wenye umri kama wangu wanafahamu, hata ngoma za utamaduni za Kitanzania akinamama hasa Wasukuma na Wagogo, wanafunga tu kwenye maziwa hapa, wanafunga na hapa chini, huku chini inakuwa kivutio. Sasa mbona hii miziki ya sasa hivi wanaleta figisu ambayo hatuwaelewi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli namwomba sana Mheshimiwa Waziri ajitahidi kukaa na wasanii, asitumie muda mwingi sana kufunga, ni bora kutumia muda mwingi kuwafundisha na kukemea yale mambo madogo madogo ili hii tasnia iendelee. Wanaona wanamsumbua Diamond hapa masikini wa Mungu, wanaona yaliyofanyika Kenya? Wenzenu wamempokea, wanamwambia imba kila kitu ulichozuiliwa. Wamempa kiwanja, wamempangia nyumba. Tutapoteza hizi bahati tubaki kung’ang’ana na mipira ambayo imeshakuwa kichwa cha mwendawazimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwulize Mheshimiwa Waziri kidogo atakapokuja kuhitimisha anisaidie. Waganga wa Kienyeji kule vijijini, ukiwa Wilayani Halmashauri wako chini ya Afisa Utamaduni. Naamini Waganga wa Kienyeji ni watu wazuri sana, tumeshindwa tu jinsi gani ya kuwatumia. Kwa kuwa Mhehimiwa Rais ameanza utaratibu wa kutoa tuzo kwa wale waliovumbua vitu, nadhani hata huku kwa Waganga wa Kienyeji aingie kidogo ili aone mambo yalivyo. Shida iliyoko, kwa nini wanawazuia kufanya matangazo wakati Wazungu wakileta chanjo za Polio wanawaruhusu watangaze kwenye…. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)