Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kuunga mkono hoja iliyotolewa yako mengi ambayo yamesemwa. Lakini kwa ajili muda nitaomba nijikite katika maeneo mawili ambayo Waheshimiwa Wabunge walipata fursa ya kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la kwanza ambalo naomba nianze ni suala zima la TARURA. Waheshimiwa Wabunge wengi sana wamechangia wengine wakiounga mkono TARURA uwanzishwaji walio wengi wameounga mkono uanzishwaji. Lakini ambalo limejirudia mara nyingi sana kwa kila Mbunge ambaye alipata fursa ya kuchangia kuhusiana na chombo hiki ni suala la mgawanyo asilimia 30 kwa 70.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulitoa ufafanuzi wakati tunahitimisha hoja ya bajeti ya kwetu lakini kwa sababu chombo hiki kinaingiliana na TANROADS ndiyo maana na leo imekuwa likijirudia mawazo ambayo yanatolewa na Waheshimiwa Wabunge inaonesha jinsi ambavyo tuna kiu ya maendeleo kuhakikisha kwamba barabara zetu na hasa zile za vijijini zinapitika vipindi vyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Serikali tunakiri, lakini pia si busara sana tukasema tunagawana umaskini kwa sababu mtandao wa barabara ambazo zinahitaji kujengwa kwa kiwango cha lami ni nyingi na kila Mbunge ambaye amepata nafasi ya kusimama hapa aliomba barabara kiwango cha lami na hata kwako nimesikia upande wa kule wakati Mheshimiwa Frank Mwakibete anasema amesema na yeye anaomba barabara ya lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, suala la kujenga barabara zetu kwa kiwango cha lami bado uhitaji ni mkubwa sana ni vizuri mkatupa fursa tukalichukua wazo jema kama hili ili tuje na namna ambayo itasaidia kuhakikisha kwamba hatuendi kufifisha kazi nzuri ambayo imeanzishwa juu ya suala zima la kujenga barabara zetu kuziunganisha zile za Mikoa na zile za mipakani kwa kiwango cha lami eti tu kwa sababu tunataka kuongezea asilimia nyingi kwenda TARURA. Ni vizuri na tukaanza kufikiria sisi Wabunge kwa ujumla wetu namna mzuri ya kupata chanzo kingine ilikuwa ni kusema kwamba sasa tunaenda kubadilisha formula kutoka asilimia 30 na 70.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna hoja ambayo imesemwa kwa urefu sana na ikawa inavuta hisia za Waheshimiwa Wabunge na hasa Wabunge wa kutoka Mkoa wa Morogoro na hoja hii iliibuliwa ikasemwa kwa uzuri sana na Mheshimiwa Devotha Minja. Sisi kama Serikali jambo hili tunalijua, lakini ni vuzri pia tukaelezana unaposema unajenga barabara kiwango cha lami tukubaliane hiyo barabara inajengwa kwa utaratibu upi na ni lami ipi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ziko aina nyingi za lami hasa katika mradi ambao umeendeshwa na unaendela tunategemea kwamba utakamilika ndani ya mwezi huu, Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa Mikoa ambayo kwa maana ya mji wa Morogoro ni mioungoni mwa miji ambayo imepata miradi huu mradi unaitwa ULGSP ambao unajengwa kwa jumla ya shilingi bilioni 12 ambao Waheshimiwa Wabunge hasa wa Morogoro walikuwa wanasema kwamba ni gharama sana kujenga barabara hii inafika mpaka bilioni tatu haijapata kutokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli haijapata kutokea, lakini hiyo barabara inajengwaje ndiyo suala ambalo lazima tuulizane. Barabara inapojengwa kuna hii inaitwa surface dressing, lakini ile ambayo tunajenga Morogoro inaitwa asphalt concrete ni miongoni mwa ujenzi wa barabara za lami ambazo zina gharama kubwa lakini ni vizuri pia tukaambizana ni kazi zipi ambazo zinafanyika. Barabara zile za Morogoro zinahusisha kilomita 4.6 na kazi ambazo zinafanyika naomba kwa ruhusa yako nizitaje. Kuna kutengeneza barabara ya Tubuyu - Nanenane Maelewano yenye urefu wa kilometa 4.6 na kazi zifuatazo zinafanyika:-

(i) Kutayarisha road bed, kuandaa matabaka ya barabara ambayo ni G3, G7, G15 na C1 kwa maana ya cement stabilizer layer; na

(ii) Kujenga njia za chini za ardhi kupitisha huduma kwa maana ya service dacks.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa mashuhuda, inapotokea barabara imejengwa mtu anataka kupitisha mabomba anakwenda kuomba kibali eti aje aanze kukata barabara, sasa kwa barabara inayojengwa Morogoro jambo hilo halitatokea kwa sababu hiyo service imeshakuwa provided. Lakini kama hiyo haitoshi, kuna kuondoa tabaka la udongo pale Morogoro ilibidi kuondoa milimita 600 kwa sababu kuna ule udongo mweusi. Kwa ujumla naomba kwa ajili ya muda niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge hakuna senti tano ambayo imeliwa na Tume zimeundwa, TAKUKURU wameenda wamechunguza ukiitazama unaweza ukadhani kwamba pesa imeliwa lakini kwa sababu ni kitu ambacho ni technical, naomba nilihakikishie Bunge lako kwamba ni thamani ya pesa imetumika Mheshimiwa Mbunge asiwe na shaka juu ya hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa muda.