Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa mchango wangu wa maandishi. Naomba kusema mkakati wa makundi uliochukuliwa na Wizara hii ya Ujenzi ili kuondo kero ya mafuriko katika jiji la Dar es Salaam. Nakushukuru kwa Wizara kuanza ujenzi wa barabara ya Kitunda, Kivule kilometa 3.2 kwa kiwango cha lami. Barabara hii huyu mkandarasi amegeuka kero kwa kwenda taratibu sana tena wakati huu na mvua hali ni mbaya sana. Pamoja na kazi nzuri ya Meneja wa TANROADS naomba Wizara iingilie kati ili kuondoa kero ya barabara hii ili kuleta ufanisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuipongeza Wizara kwa kuongeza kilometa tano za Kivule - Msongola ila naomba huyu mkandarasi asipate tena kazi kwa sababu ni mharibifu na anaichafua Serikali (SAI na TANG Co.)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Pugu inahitaji mipango mikubwa ya kuipanua ili ikidhi kiwango na wakati kwa idadi ya watu waliopo. Barabara ya Chanika - Mbande ni kero kubwa hasa kwa daraja lilikatika na mashimo makubwa barabarani. Naomba Wizara iharakishe ujenzi wa barabara ya Pugu - Kinyerezi - Kifuru ili kupunguza mzunguko wa wananchi wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.