Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, niombe na nichangie kwanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo. Naomba nichangie Wizara hii muhimu kwanza kwa kuwapongeza Waziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wote pamoja na wasaidizi wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishauri kwanza kuiomba Serikali iondoe kodi kwenye mitambo ya kutengeneza barabara lakini pia utasaidia katika sekta ya maji kwenye mabwawa. Kodi itozwe kwenye kazi na siyo kwenye kuingiza mitambo pia kuondoa kodi kwenye miradi yenye maslahi ya kitaifa na ya kijamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri pia Wizara kupitia Serikali iangalie namna ya kuhakikisha suala la NEMC - utafiti wa mazingira katika suala la minara ya simu. Miradi mingi hukwama kwa ajili ya Environmental Impact Assessment (ripoti ya masuala ya mazingira). Serikali iangalie namna ya kuboresha mawasiliano hasa data ili twende na teknolojia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipongeze, ushauri wangu wa kuendelea kutumia taasisi za kwetu kama TTCL kwa shughuli za Serikali. Kazi yao sasa ni nzuri sana na tuendelee kuboresha kwa kuwekeza.

Naomba pia tuangalie namna ya kuboresha mapato kupitia mitandao hasa utumiaji wa simu za ndani na hasa fedha zinazopitishwa humo. Sim Banking leo hii hatupati mapato ya sekta hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nashauri Wizara iwekeze kwenye viwanja vya ndege na bandari, zaidi huduma za kuhifadhi bidhaa ya kilimo, mifugo na uvuvi kwa kuwa na cold rooms. Huduma za kuwekeza bidhaa hizo kwa hali ya hewa inayoweza kuratibiwa uwanja wa KIA inahitaji kwa haraka huduma hiyo kwa ajili ya kusafirisha maua na mboga mboga.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.