Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wizara nzima kwa kazi nzuri ya kusaidia kuweka miundombinu wezeshi ya kukuza uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Wilaya ya Karagwe barabara ya Nyakahanga – Nyakakika (kilometa 96) imekasimishwa TANROADS (2017/2018) na ilitengewa shilingi milioni 150. Fedha hizi ni kidogo mno ukilinganisha na ukorofi wa barabara. Financial year 2018/2019 imetengwa hiyo hiyo shilingi milioni 150, ninasikitika hii fedha haitaweza kutosha maeneo yote korofi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi, barabara hii ni korofi sana naomba iongezewe fedha; ahadi ya kilometa tano za lami kwenda eneo korofi zaidi la Kajura Nkeito naomba itimizwe, eneo hili lipo barabara hii tajwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Bugene – Benako ni financial year ya pili bajeti zinatenga hewa kwa ajili ya kujenga kwa kiwango cha lami, kwa nini? Je, wananchi wa hii barabara watalipwa lini fidia zao? Detailed design imekamilika.


Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mugakorongo – Marongo kwa nini detailed design yake inachukua muda mrefu na wakati barabara hii ikiunganishwa na ile ya Bugene – Benako zinaunganisha Afrika Mashariki na kukamilika kwake kutachochea uchumi wa Kagera na nchi yetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Wizara iongeze bajeti ya TARURA kwani hizi feeder roads za vijiji ndizo tunazitegemea kusafirisha mazao ya wakulima, wafugaji na wafanyabiashara wadogo kwenye kuzalisha uchumi wa kaya na nchi. Ratio ya mgao iwe angalau 40/60 minimum. Ideally ration iwe 45/55.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee namshukuru sana Meneja wangu wa TANROADS Mkoa, Engineer Kasamwa kwa kazi nzuri ya kusimamia kazi za mkoa na kwa ushirikiano anaonipa. Ni matumaini yangu maombi yangu yatakubaliwa. Nawatakia majukumu mema. Ahsante.