Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kukumbushia ahadi za viongozi wakuu zifuatazo ambazo utekelezaji wake haujaanza Wilayani Misenyi, Jimbo la Nkenge.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya lami ya Katoma hadi Bukwali; barabara ya lami Kajai – Hospitali ya Magana (Hospitali Teule ya Wilaya); barabara ya lami ya Matukula hadi Minziro; barabara ya lami ya Kituo cha Afya Kabyaile hadi Gera; kilometa tatu za lami Makao Makuu ya Wilaya – Bunazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa muda mrefu Serikali ilisimamisha shughuli za maendeleo katika eneo la Kajunguti. Baada ya Serikali kufanya maamuzi ya kutojenga tena Uwanja wa Ndege – Kajunguti ni dhahiri wananchi walioacha kuendeleza maeneo yao ya Kajunguti watakuwa wamepata hasara kubwa. Naomba Serikali iangalie uwezekano wa kuwapa chochote wananchi kufidia hasara waliyoipata.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.