Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kivuko cha MV Nyerere kimekuwa na matatizo ya mara kwa mara ya kuzimika katikati ya maji hali inayohatarisha maisha ya abiria, kwa mara ya mwisho nilipewa taarifa kuwa engine za kivuko hiki zingekamilika na kufungwa kabla ya mwezi Februari lakini sioni kinachoendelea. Ni lini engine za kivuko cha MV Nyerere zitafungwa na kuondoa kero ya usafiri kati ya Bugorola na Ukara?

Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira ya usafiri kati ya Kisiwa cha Irugwa na Ukerewe ni ya hatari kutokana na ukweli kwamba inahitajika zaidi ya masaa manne kwa abiria kusafiri kati ya visiwa hivi viwili wakitumia mitumbwi jambo ambalo ni hatari. Ombi langu kwa Serikali itafakari na kusaidia upatikanaji wa usafiri wa boti/kivuko kati ya Irugwa kwenye wakazi zaidi ya 20,000 na Ukerewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu malipo kwa watumishi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), baada ya kampuni hii kudorora na meli nyingi kushindwa kufanya kazi, wafanyakazi wa kampuni hii hawajalipwa mishahara kwa miezi 23 jambo lisilo na afya. Serikali itumie vyombo vyake kubaini watumishi walio na matatizo waondolewe na wale waadilifu walipwe haki yao na hivyo kuongeza morali ya utendaji kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro ya nauli katika vivuko; utaratibu wa jumla kutoza kiwango fulani cha pesa kwa mizigo chini ya kilo 20 umekuwa na migogoro ya mara kwa mara kwa sababu wananchi wamekuwa wananyanyasika kwa kutozwa nauli kwa mizigo isiyostahili kama vile mabegi na vitu vingine vidogo vidogo ambavyo havistahili, hivyo, napendekeza malipo yoyote yaondolewe kwa mizigo ya chini ya kilo 20.