Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ujenzi wa barabara ya Itoni – Manda yenye urefu wa kilometa 211. Ujenzi wa kiwango cha zege kati ya Lusitu na Mawengi unasuasua sana. Naishauri Serikali kwamba barabara hii ipo ndani ya majimbo mawili au Wilaya mbili kwa maana ya Wilaya ya Njombe na Wilaya ya Ludewa na kazi imeanza ndani ya Wilaya ya Ludewa na kuruka kipande cha kilometa 52 kilichopo Wilaya ya Njombe ambacho ndicho kinaunga kwenye barabara kuu ya Makambako - Songea eneo la Itoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa pesa kidogo inayotenga kwa barabara hii, sasa iajiri mkandarasi mwingine aanzie Itoni ili kuweka imani kwa wananchi wa eneo la Jimbo la Njombe Mjini kwani ahadi ya lami kutoka Itoni ni ya muda mrefu sana.