Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, upgrading of Sumbawanga – Namanyere–Mpanda Road, package 3; Kizi – Lyambalyamfipa – Sitalike Section 86.5 kilometres.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanikiwa kwa asilimia kubwa package I & II na sasa wananchi wanatumia barabara hizo, lakini package III bado haijatengewa fedha katika mwaka wa fedha 2018/2019 kiwango cha lami ambapo kilometa 35.5 kati ya kilometa 86.5 hazipo katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi. Naomba Waziri atuambie wananchi wa Katavi ni lini fedha zitatengwa kwa ajili ya kipande hicho cha kilometa 35.5?

Mheshimiwa Naibu Spika, kupandishwa hadhi barabara ya Katumba Complex II (Msaginya – Mnyaki – Kanoge kilometa 21) Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo (Katavi). TARURA wameomba barabara hii ipande hadhi kuwa chini ya TANROADS kwa kuwa ni muhimu sana na ni kiunganishi cha barabara mbili zinazotoka nje ya Mkoa wa Katavi ambazo ni Mpanda – Ugala – Ulyankulu, Kaliua – Kahama kilometa 457 na Mpanda – Ipele – Tabora (kilometa 346).

Mheshimiwa Naibu Spika, reli Mpanda – Tabora, bado hali ni mbaya sana njia ya reli Mpanda – Tabora hususani kipande cha Kaliua – Mpanda, mpaka abiria walilala njiani siku mbili baada ya mvua kufanya uharibifu, ilikuwa tarehe 18/04/2018 waliondoka Tabora na walifika Mpanda tarehe 20/04/2018 saa 12 asubuhi. TRL inaombwa kuongeza ukarabati wa njia kwa kuwa ni tegemeo la wananchi na kusafirisha mazao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, inakabiliwa na changamoto kubwa ya mawasiliano katika kata za Ugala, Litapunguza, Kamage, Katumba, Uvaira, Nsimbo, Mtapenda, Kapalala, Machimboni, Itanka, Ibindi na Sitalike. Tunaomba sana Serikali kuboresha mawasiliano katika kata tajwa hapo juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Soko la Hisa kwa Kampuni za Simu, Bunge lako lilipitisha sheria inayozilazimu kampuni zote za simu kujiunga na soko la hisa, lakini mpaka sasa Vodacom ndio pekee wameshajiunga. Je, ni lini kampuni nyingine zikiwemo TTCL watatekeleza matakwa ya sheria? Kwa kuwa bado kampuni zingine kutekeleza; je, sheria inasema vipi juu ya hatua za kuchukuliwa kwa kutotii sheria hizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, fidia ya matenki ya maji, mkataba wa mkandarasi Mpanda – Ipole – Tabora, anatakiwa kufidia matenki mawili ambayo thamani yake zaidi ya milioni 250 lakini fidia iliyopo ni ndogo haizidi milioni 150; kwa hiyo tunaiomba Serikali iangalie upya fidia hiyo na ikiwezekana Halmashauri ya Nsimbo ipewe fedha moja kwa moja ili ijenge yenyewe miundombinu ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, service levy V/s TCRA; Kampuni za Simu zinaingiza mapato kutokana na minara hivyo kutokana na sheria za Serikali za Mitaa wanatakiwa kutoza service levy ya asilimia 6.3 ya mapato. Tunaomba TCRA wasimamie utaratibu mzuri ili kila Halmashauri inufaike na minara iliyopo katika eneo lao au Serikali ifanye ring fence ya service levy kutoka katika kampuni zote na pato hili kuwekwa Wizara ya Afya ili kusaidia kazi za kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, fidia barabara ya Sitalike - Mpanda; bado kuna wananchi wanadai hawajalipwa na Serikali, tunaomba ifanye malipo haraka.